Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Yobu 4:17 - Swahili Revised Union Version

17 Je! Binadamu atakuwa na haki kuliko Mungu? Je! Mtu atakuwa safi kuliko Muumba wake?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

17 Binadamu afaye aweza kuwa mwadilifu mbele ya Mungu? Mtu aweza kuwa safi mbele ya Muumba wake?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

17 Binadamu afaye aweza kuwa mwadilifu mbele ya Mungu? Mtu aweza kuwa safi mbele ya Muumba wake?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

17 Binadamu afaye aweza kuwa mwadilifu mbele ya Mungu? Mtu aweza kuwa safi mbele ya Muumba wake?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

17 ‘Je, binadamu aweza kuwa mwadilifu kuliko Mungu? Je, mtu aweza kuwa safi kuliko Muumba wake?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

17 ‘Je, binadamu aweza kuwa mwadilifu kuliko Mungu? Je, mtu aweza kuwa safi kuliko Muumba wake?

Tazama sura Nakili




Yobu 4:17
25 Marejeleo ya Msalaba  

La hasha! Usifanye hivyo, ukamwue mwenye haki pamoja na mwovu, mwenye haki awe kama mwovu. Hasha! Mhukumu ulimwengu wote asitende haki?


Ni nani awezaye kutoa kitu kilicho safi kitoke katika kitu kichafu? Hapana awezaye.


Je! Mwanadamu ni kitu gani, hata akawa safi? Huyo aliyezaliwa na mwanamke, hata awe na haki?


Basi mtu awezaje kuwa na haki mbele ya Mungu? Au awezaje kuwa safi aliyezaliwa na mwanamke?


Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye? Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni?


Kwa kuwa mimi sijui kujipendekeza; Au Muumba wangu angeniondoa kwa upesi.


Wala hapana asemaye, Yuko wapi Mungu Muumba wangu, Awapaye nyimbo wakati wa usiku;


Je! Wewe wadhani kwamba haya ni haki yako, Au je! Wasema, Ni haki yangu mbele za Mungu,


Nitayaleta maarifa yangu kutoka mbali, Nami nitampa haki Muumba wangu.


Hiyo pepo ilisimama kimya, nisiweze kutambua sura zake, Mfano ulikuwa mbele ya macho yangu; Kulikuwa kimya, nami nilisikia sauti, ikinena,


Je! Hata hukumu yangu utaibatilisha? Utanitia mimi hatiani, upate kuhesabiwa haki?


Je! Mungu hupotosha hukumu? Au, huyo Mwenyezi hupotosha yaliyo ya haki?


Kweli najua kuwa ndivyo hivyo; Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu?


Wala usimhukumu mtumishi wako, Maana kwako hakuna aliye hai mwenye haki.


BWANA ni mwenye haki katika njia zake zote, Na mwenye huruma katika matendo yake yote.


Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, atendaye mema pasipo kutenda dhambi.


Wewe u mwenye haki, Ee BWANA, nitetapo nawe, lakini nitasema nawe katika habari ya haki. Mbona njia ya wabaya inasitawi? Mbona wote watendao hila wanakaa salama?


Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?


Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazieleweki!


Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu,


La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwa nini umeniumba hivi?


Na hawa wenye uhai wanne, kila mmoja alikuwa na mabawa sita; pande zote na ndani wamejaa macho, wala hawapumziki mchana wala usiku, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Bwana Mungu Mwenyezi, aliyekuwako na aliyeko na atakayekuja.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo