Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 92:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Maana hao adui zako, Ee BWANA, Hao adui zako watapotea, Na watendao maovu watatawanyika wote pia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Hao maadui zako, ee Mwenyezi-Mungu, naam, hao maadui zako, hakika wataangamia; wote watendao maovu, watatawanyika!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Hao maadui zako, ee Mwenyezi-Mungu, naam, hao maadui zako, hakika wataangamia; wote watendao maovu, watatawanyika!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Hao maadui zako, ee Mwenyezi-Mungu, naam, hao maadui zako, hakika wataangamia; wote watendao maovu, watatawanyika!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Ee Mwenyezi Mungu, hakika adui zako, hakika adui zako wataangamia. Wote watendao maovu watatawanyika.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Ee bwana, hakika adui zako, hakika adui zako wataangamia. Wote watendao mabaya watatawanyika.

Tazama sura Nakili




Zaburi 92:9
21 Marejeleo ya Msalaba  

Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.


Wewe mwenyewe utasimama, Na kuirehemu Sayuni, Kwa maana ndio wakati wa kuihurumia, Naam, majira yaliyoamriwa yamewadia.


Hapo mwanzo uliutia msingi wa nchi, Na mbingu ni kazi ya mikono yako.


Bali wasio haki watapotea, Nao wamchukiao BWANA watatoweka, Kama uzuri wa mashamba, Kama moshi watatoweka.


Usiwaue, watu wangu wasije wakasahau; Uwatawanye kwa uweza wako, Na kuwaangamiza, Ee Bwana, ngao yetu.


Mkemee mnyama wa mafunjoni; Kundi la mafahali, na ndama za watu; Hata wanyenyekee na kuleta vipande vya fedha, Uwatawanye watu wapendao vita.


Maana wajitengao nawe watapotea; Umewaangamiza wote waliokuacha Wewe.


Ndiwe uliyemponda Rahabu akawa kama aliyeuawa, Kwa mkono hodari umewatawanya wakuchukiao.


Maana Wewe, BWANA, ndiwe Uliye juu, Juu sana kuliko nchi yote; Umetukuka sana juu ya miungu yote.


Mataifa wananguruma kama ngurumo ya maji mengi; Lakini atawakemea, nao watakimbia mbali sana, Watafukuzwa kama makapi milimani mbele ya upepo, Na kama mavumbi vuruvuru mbele ya tufani.


Theluthi yenu mtakufa kwa tauni, na kwa njaa watakomeshwa ndani yako; na theluthi yenu wataanguka kwa upanga pande zako zote; na theluthi yenu nitawatawanya kwa pepo zote, kisha nitafuta upanga nyuma yao.


Nanyi nitawatapanyatapanya katika mataifa, nami nitaufuta upanga nyuma yenu; na nchi yenu itakuwa ni ukiwa, na miji yenu maganjo.


Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee BWANA, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao.


Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.


Tena, wale adui zangu, wasiotaka niwatawale, waleteni hapa muwachinje mbele yangu.


Wataanguka kwa ukali wa upanga, nao watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote; na Yerusalemu utakanyagwa na Mataifa, hadi majira ya Mataifa yatakapotimia.


BWANA atakutawanya katika mataifa yote, tokea ncha hii ya dunia hata ncha hii ya dunia; nawe huko utatumikia miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako, nayo ni miti na mawe.


Na waangamie vivyo hivyo adui zako wote, Ee BWANA. Bali wao wampendao na wawe kama jua hapo litokapo kwa nguvu zake. Nayo nchi ikastarehe miaka arubaini.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo