Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 92:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

3 Kwa chombo chenye nyuzi kumi, Na kwa kinanda, Na kwa mlio wa kinubi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 kwa muziki wa zeze na kinubi, kwa sauti tamu ya zeze.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 kwa muziki wa zeze na kinubi, kwa sauti tamu ya zeze.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 kwa muziki wa zeze na kinubi, kwa sauti tamu ya zeze.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 kwa zeze yenye nyuzi kumi na kwa sauti ya kinubi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 kwa zeze yenye nyuzi kumi na kwa sauti ya kinubi.

Tazama sura Nakili




Zaburi 92:3
17 Marejeleo ya Msalaba  

Wakacheza Daudi na Israeli wote, mbele za Mungu, kwa nguvu zao zote; na kwa nyimbo na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa matoazi, na kwa tarumbeta.


Kisha Daudi akamwambia mkuu wa Walawi, kwamba awaagize ndugu zao waimbaji, pamoja na vyombo vyao vya kupigia ngoma, vinanda, na vinubi, na matoazi, wavipige na kupaza sauti kwa furaha.


nao wasimame kila asubuhi kumshukuru na kumsifu BWANA, na jioni vivyo hivyo;


Hao wote waliamriwa na baba yao, waimbe nyumbani mwa BWANA, wakiwa na matoazi, vinanda, na vinubi, kwa utumishi wa nyumba ya Mungu; Asafu, Yeduthuni, na Hemani wakiwa wanaamriwa na mfalme.


Wakafika Yerusalemu wenye vinanda, vinubi na parapanda kwenda nyumbani kwa BWANA.


na theluthi nyumbani pa mfalme; na theluthi langoni pa msingi; na watu wote watakuwapo nyuani mwa nyumba ya BWANA.


Akawasimamisha Walawi nyumbani mwa BWANA wenye matoazi, wenye vinanda, na wenye vinubi, kama alivyoamuru Daudi, na Gadi mwonaji wa mfalme, na Nathani nabii; kwani BWANA aliamuru hivi kwa manabii wake.


Basi, walipouweka wakfu ukuta wa Yerusalemu wakawatafuta Walawi katika mahali pao pote, ili kuwaleta Yerusalemu, ili waweze kusherehekea kuweka wakfu pamoja na furaha, na kwa shukrani, na kwa kuimba, kwa matoazi, vinanda na vinubi.


Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa sauti tamu ya matari na kinubi.


Mshukuruni BWANA kwa kinubi, Kwa kinanda cha nyuzi kumi mwimbieni sifa.


Nitamwambia Mungu, mwamba wangu, Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?


Amka, ee moyo wangu. Amka, kinanda na kinubi, Nitaamka alfajiri.


Waimbaji hutangulia, nyuma yao wapigao vinanda, Kati ya wanawali wapiga matari.


BWANA amejidhihirisha na kutekeleza hukumu; Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake.


Baada ya hayo utafika Gibea ya Mungu, hapo palipo na ngome ya Wafilisti; kisha itakuwa, utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakishuka kutoka mahali pa juu, wenye kinanda, na tari, na kinubi, na filimbi mbele yao, nao watakuwa wakitabiri;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo