Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 92:14 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

14 Watazaa matunda hadi wakati wa uzee, Watajaa utomvu, watakuwa na ubichi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

14 huendelea kuzaa matunda hata uzeeni; daima wamejaa utomvu na wabichi;

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

14 huendelea kuzaa matunda hata uzeeni; daima wamejaa utomvu na wabichi;

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

14 huendelea kuzaa matunda hata uzeeni; daima wamejaa utomvu na wabichi;

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

14 Wakati wa uzee watakuwa bado wanazaa matunda, watakuwa wabichi tena wamejaa nguvu,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

14 Wakati wa uzee watakuwa bado wanazaa matunda, watakuwa wabichi tena wamejaa nguvu,

Tazama sura Nakili




Zaburi 92:14
13 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini mwenye haki ataishika njia yake, Naye mwenye mikono safi atazidi kupata nguvu.


Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.


Na hata nikiwa ni mzee mwenye mvi, Ee Mungu, usiniache. Hata niwaeleze watu wa kizazi hiki nguvu zako, Na kila atakayekuja uweza wako.


Bali njia ya wenye haki ni kama nuru ing'aayo, Ikizidi kung'aa hata mchana mkamilifu.


na hata uzee wenu mimi ndiye, na hata wakati wenu wa mvi nitawachukueni; nimefanya, nami nitachukua; naam, nitachukua na kuokoa.


Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa joto ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda.


Na karibu na mto, juu ya ukingo wake, upande huu na upande huu, utamea kila mti wa chakula, ambao majani yake hayatanyauka, wala matunda yake hayataisha kamwe; utatoa matunda mapya kila mwezi, kwa sababu maji yake yanatoka mahali patakatifu; na matunda yake yatakuwa ni chakula; na majani yake yatakuwa ni dawa.


Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.


akiwa mmejazwa matunda ya haki, kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa ya Mungu.


Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung'olewa kabisa;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo