Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 89:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

7 Mungu huogopwa sana barazani pa watakatifu, Ni wa kuhofiwa kuliko wote wanaomzunguka.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Wewe waogopwa katika baraza la watakatifu; wote wanaokuzunguka wanatiwa hofu kuu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Wewe waogopwa katika baraza la watakatifu; wote wanaokuzunguka wanatiwa hofu kuu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Wewe waogopwa katika baraza la watakatifu; wote wanaokuzunguka wanatiwa hofu kuu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana, anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana, anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka.

Tazama sura Nakili




Zaburi 89:7
17 Marejeleo ya Msalaba  

Ni nani aliye mfano wa BWANA, Mungu wetu aketiye juu;


Mpeni BWANA, enyi wana wa Mungu, Mpeni BWANA utukufu na nguvu;


Kwa kuwa BWANA Aliye Juu, mwenye kuogofya, Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote.


Katikati ya miungu hakuna kama Wewe, Bwana, Wala matendo mfano wa matendo yako.


Basi, mtamlinganisha Mungu na nani? Au mtamfananisha na mfano wa namna gani?


Mtanifananisha na nani, basi, nipate kuwa sawa naye? Asema yeye aliye Mtakatifu.


Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.


Bali BWANA ndiye Mungu wa kweli; Ndiye Mungu aliye hai, Mfalme wa milele; Mbele za ghadhabu yake nchi yatetemeka, Wala mataifa hawawezi kustahimili hasira yake.


Ni nani asiyekucha wewe, Ee mfalme wa mataifa? Maana hii ni sifa yako wewe; kwa kuwa miongoni mwa wenye hekima wote wa mataifa, na katika hali yao ya enzi yote pia, hapana hata mmoja kama wewe.


Ndipo Musa akamwambia Haruni, Jambo hili ni hilo BWANA alilolinena, akisema, Nitatakaswa mimi katika hao wanikaribiao, nami nitatukuzwa mbele ya watu hao wote. Haruni akanyamaza kimya.


Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika Jehanamu.


Hofu nyingi ikalipata kanisa lote na watu wote walioyasikia haya.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo