Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 89:38 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

38 Lakini wewe umemtupa na kumkataa, Umemghadhibikia masihi wako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

38 Lakini sasa ee Mungu, umemtupa na kumkataa, umejaa ghadhabu dhidi ya huyo uliyemweka wakfu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

38 Lakini sasa ee Mungu, umemtupa na kumkataa, umejaa ghadhabu dhidi ya huyo uliyemweka wakfu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

38 Lakini sasa ee Mungu, umemtupa na kumkataa, umejaa ghadhabu dhidi ya huyo uliyemweka wakfu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

38 Lakini wewe umemkataa, umemdharau, umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

38 Lakini wewe umemkataa, umemdharau, umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 89:38
19 Marejeleo ya Msalaba  

Enyi milima ya Gilboa, visiwepo juu yenu Umande wala mvua, wala mashamba ya matoleo; Maana ndipo ilipotupwa kwa aibu ngao ya shujaa, Ngao yake Sauli, pasipo kutiwa mafuta.


lakini akisema kama hivi, Mimi si radhi nawe kabisa; basi, mimi hapa, na anitendee kama aonavyo kuwa vyema.


Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa BWANA huchunguza mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, atakuwa nawe; ukimwacha, atakutupa milele.


Hasira ya BWANA ikawaka juu ya watu wake, Akauchukia urithi wake.


Ee Mungu, umetutupa na kututawanya, Umekuwa na hasira, uturudishe tena.


Ee Mungu, si Wewe uliyetutupa? Wala, Ee Mungu, hutoki na majeshi yetu?


Je! Bwana atatutupa milele na milele? Asiwe na fadhili kwetu kamwe?


Mungu alisikia, akaghadhibika, Akamkataa Israeli kabisa.


Ee Mungu, ngao yetu, uangalie, Umtazame uso masihi


Ambayo adui zako wamesimanga, Ee BWANA, Naam, wamezisimanga hatua za masihi wako.


Wewe u mwenye haki, Ee BWANA, nitetapo nawe, lakini nitasema nawe katika habari ya haki. Mbona njia ya wabaya inasitawi? Mbona wote watendao hila wanakaa salama?


Bwana ameitupilia mbali madhabahu yake, Amepachukia patakatifu pake; Amezitia katika mikono ya hao adui Kuta za majumba yake; Wamepiga kelele ndani ya nyumba ya BWANA Kama katika sikukuu.


Pumzi ya mianzi ya pua zetu, masihi wa BWANA, Alikamatwa katika marima yao; Ambaye kwa habari zake tulisema, Chini ya kivuli chake tutakaa kati ya mataifa.


Mungu wangu atawatupilia mbali, kwa sababu hawakumsikiliza; nao watakuwa watu wa kutangatanga kati ya mataifa.


Nami nikawakatilia mbali wachungaji watatu katika mwezi mmoja; maana nafsi yangu ilikuwa imechoka kwa ajili yao, na nafsi zao pia walinichukia.


Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu, na juu ya mtu aliye mwenzangu, asema BWANA wa majeshi; mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika; nami nitaugeuza mkono wangu juu ya wadogo.


BWANA akaona, akawachukia, Kwa sababu ya kukasirishwa na wanawe na binti zake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo