Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 89:29 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

29 Wazao wake nao nitawadumisha milele, Na kiti chake cha enzi kama siku za mbingu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

29 Nitaudumisha daima ukoo wake wa kifalme, na ufalme wake kama mbingu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

29 Nitaudumisha daima ukoo wake wa kifalme, na ufalme wake kama mbingu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

29 Nitaudumisha daima ukoo wake wa kifalme, na ufalme wake kama mbingu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

29 Nitaudumisha uzao wake milele, kiti chake cha utawala kama mbingu zinavyodumu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

29 Nitaudumisha uzao wake milele, kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.

Tazama sura Nakili




Zaburi 89:29
16 Marejeleo ya Msalaba  

Je! Sivyo ilivyo nyumba yangu mbele za BWANA? Kwa kuwa amefanya nami agano la milele; Ina taratibu katika yote, ni thabiti, Maana ni wokovu wangu wote, na shauku langu lote.


huyo ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu; naye atakuwa mwanangu, nami nitakuwa babaye; nami nitakiimarisha milele kiti cha ufalme wake juu ya Israeli.


BWANA amemwapia Daudi neno la kweli, Hatarudi nyuma akalivunja, Mmoja wa wazawa wako mwenyewe Nitawaweka katika kiti chako cha enzi.


Alikuomba uhai, ukampa, Muda mrefu wa siku nyingi, milele na milele.


Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.


Wazawa wake watadumu milele, Na kiti chake cha enzi kuwa mbele yangu kama jua.


Wazao wako nitawaimarisha milele, Nitakijenga kiti chako cha enzi hata milele.


Tegeni masikio yenu, na kunijia; Sikieni, na nafsi zenu zitaishi; Nami nitafanya nanyi agano la milele, Naam, rehema za Daudi zilizo imara.


Tena kuhusu habari zangu, hili ndilo agano langu nao, asema BWANA; roho yangu iliyo juu yako, na maneno yangu niliyoyatia kinywani mwako, hayataondoka kinywani mwako, wala kinywani mwa wana wako, wala kinywani mwa wajukuu wako, asema BWANA, tangu leo na hata milele.


Mamlaka ya enzi yake yatakuzwa daima, Na kutakuwa na amani isiyo na mwisho, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa BWANA wa majeshi ndio utakaotenda hayo.


Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.


ili siku zenu zifanywe nyingi, na za vijana vyenu nao, juu ya nchi BWANA aliyowaapia baba zenu kuwa atawapa, kama zilivyo siku za mbingu juu ya nchi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo