Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 88:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

12 Miujiza yako itajulikana gizani? Au haki yako katika nchi ya usahaulifu?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

12 Je, maajabu yako yanajulikana humo gizani, au wema wako katika nchi ya waliosahauliwa?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

12 Je, maajabu yako yanajulikana humo gizani, au wema wako katika nchi ya waliosahauliwa?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

12 Je, maajabu yako yanajulikana humo gizani, au wema wako katika nchi ya waliosahauliwa?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?

Tazama sura Nakili




Zaburi 88:12
10 Marejeleo ya Msalaba  

Maana adui ameifuatia nafsi yangu, Ameutupa chini uzima wangu. Amenikalisha mahali penye giza, Kama watu waliokufa zamani.


Nimesahauliwa kama mfu asiyekumbukwa; Nimekuwa kama chombo kilichovunjika.


Miongoni mwao waliokufa nimetupwa, Kama waliouawa walalao makaburini. Hao ambao Wewe huwakumbuki tena, Wametengwa mbali na mkono wako.


Maana hakuna kumbukumbu la milele la mwenye hekima, wala la mpumbavu; kwa sababu siku zijazo wote pia watakuwa wamekwisha kusahauliwa. Na mwenye hekima, jinsi gani anavyokufa sawasawa na mpumbavu!


Pia nikaona waovu wamezikwa, nao wamefika kaburini; tena waliofanya mema wameondoka katika patakatifu, nao wamesahauliwa mjini. Hayo nayo ni ubatili.


kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lolote, wala hawana tuzo tena; maana hata kumbukumbu lao limesahauliwa.


nao wataiangalia nchi, na, tazama, shida na giza; hapatakuwa changamko kwa sababu ya dhiki; nao watafukuzwa na kuingia katika giza kubwa.


bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.


ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo