Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 86:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

8 Katikati ya miungu hakuna kama Wewe, Bwana, Wala matendo mfano wa matendo yako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Ee Bwana, hakuna Mungu aliye kama wewe; hakuna awezaye kufanya unayofanya wewe.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Ee Bwana, hakuna Mungu aliye kama wewe; hakuna awezaye kufanya unayofanya wewe.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Ee Bwana, hakuna Mungu aliye kama wewe; hakuna awezaye kufanya unayofanya wewe.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Ee Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe, hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Ee bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe, hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 86:8
16 Marejeleo ya Msalaba  

Angalia, najenga nyumba kwa jina la BWANA, Mungu wangu, ili kumfanyia wakfu, ya kufukizia mbele zake fukizo la manukato, na ya mkate wa wonyesho wa daima, na ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na jioni, na za siku za sabato, na za mwezi mpya, na za sikukuu zilizoagizwa za BWANA, Mungu wetu. Hili ni agizo la milele kwa Israeli.


Maana najua ya kuwa BWANA ni mkuu, Na Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.


Yeye peke yake afanya maajabu makuu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.


Maana ni nani katika mbingu awezaye kulinganishwa na BWANA? Ni nani afananaye na BWANA miongoni mwa malaika?


Mungu huogopwa sana barazani pa watakatifu, Ni wa kuhofiwa kuliko wote wanaomzunguka.


BWANA, Mungu wa majeshi, Ni nani aliye hodari kama Wewe, Ee YAHU? Na uaminifu wako unakuzunguka.


Kwa kuwa BWANA ni Mungu mkuu, Na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.


Ee BWANA, katika miungu ni nani aliye kama wewe? Ni nani aliye kama wewe, mtukufu katika utakatifu, Mwenye kuogopwa katika sifa zako, mfanya maajabu?


Basi Haruni akaunyosha mkono wake juu ya maji yote ya Misri; na hao vyura wakakwea juu, wakaifunika nchi ya Misri.


Basi, mtamlinganisha Mungu na nani? Au mtamfananisha na mfano wa namna gani?


Mtanifananisha na nani, basi, nipate kuwa sawa naye? Asema yeye aliye Mtakatifu.


Yeye, Fungu la Yakobo, siye kama hawa; Maana ndiye aliyeviumba vitu vyote; Na Israeli ni kabila la urithi wake; BWANA wa majeshi ndilo jina lake.


Basi mimi naweka amri ya kuwa kila kabila la watu, na kila taifa, na kila lugha, watakaonena neno lolote lisilopasa juu ya huyo Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego, watakatwa vipande vipande, na nyumba zao zitafanywa jaa; kwa kuwa hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.


Ee BWANA Mungu, umeanza kumwonesha mtumishi wako ukubwa wako, na mkono wako wa nguvu; kwani kuna mungu gani mbinguni au duniani awezaye kufanya mfano wa kazi zako, na mfano wa matendo yako yenye nguvu?


Au Mungu amekwenda wakati gani akajitwalia taifa kutoka kati ya taifa lingine, kwa majaribu, ishara, maajabu, vita, mkono hodari, mkono ulionyoshwa, na vitisho vikuu, kama vile BWANA, Mungu wenu, alivyowatendea ninyi katika Misri, mbele ya macho yenu?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo