Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 85:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Hakika wokovu wake uko karibu na wamchao, Ndipo utukufu wake ukae katika nchi yetu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Hakika yu tayari kuwaokoa wanaomheshimu, na utukufu wake utadumu nchini mwetu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Hakika yu tayari kuwaokoa wanaomheshimu, na utukufu wake utadumu nchini mwetu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Hakika yu tayari kuwaokoa wanaomheshimu, na utukufu wake utadumu nchini mwetu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Hakika wokovu wake uko karibu na wale wamchao, ili utukufu wake udumu katika nchi yetu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Hakika wokovu wake uko karibu na wale wamchao, ili utukufu wake udumu katika nchi yetu.

Tazama sura Nakili




Zaburi 85:9
22 Marejeleo ya Msalaba  

Wokovu u mbali na wasio haki, Kwa maana hawajifunzi amri zako.


Atoaye dhabihu za kushukuru, Ndiye anayenitukuza. Naye autengenezaye mwenendo wake, Nitamwonesha wokovu wa Mungu.


Tena juu ya makao yote ya mlima Sayuni, na juu ya makusanyiko yake, BWANA ataumba wingu na moshi wakati wa mchana, na mwangaza wa miali ya moto wakati wa usiku; kwa maana juu ya utukufu wote itatandazwa sitara.


Mimi ninaleta karibu haki yangu, haitakuwa mbali, na wokovu wangu hautakawia; nami nitaweka wokovu katika Sayuni kwa ajili ya Israeli, utukufu wangu.


Mtasema hivi kila mtu na jirani yake, na kila mtu na ndugu yake, BWANA amejibu mtu? Na, BWANA amesemaje?


Nawe utamwambia nabii hivi, BWANA amekujibu nini? Na, BWANA amesemaje?


Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za baadaye.


ndipo nitakapokushusha pamoja nao washukao shimoni, uende kwa watu wa kale; nami nitakukalisha pande za chini za nchi; mahali palipokuwa ukiwa tangu zamani, pamoja nao washukao shimoni; ili usikaliwe na watu, wala usiweke utukufu wako katika nchi yao walio hai.


Tena akaniambia, Mwanadamu, maneno yangu yote nitakayokuambia, yapokee moyoni mwako, na kuyasikia kwa masikio yako.


Mimi nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara, nitaangalia ili nione atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu kuhusu kulalamika kwangu.


Kwa maana mimi, asema BWANA, nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka pande zote, nami nitakuwa huo utukufu ndani yake.


Kwa maana BWANA wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake.


Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli.


Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.


Mtu akipenda kuyatenda mapenzi yake, atajua habari ya yale mafunzo, kwamba yatoka kwa Mungu, au kwamba mimi nanena kwa nafsi yangu tu.


Paulo akasimama, akawapungia mkono, akasema, Enyi Waisraeli, nanyi mnaomcha Mungu, sikilizeni.


Kwa hiyo Eli akamwambia Samweli, Nenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena, BWANA; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo