Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 85:6 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

6 Je! Hutaki kurudi na kutuhuisha, Ili watu wako wakufurahie?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 Je, hutatujalia tena maisha mapya, ili watu wako wafurahi kwa sababu yako?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 Je, hutatujalia tena maisha mapya, ili watu wako wafurahi kwa sababu yako?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 Je, hutatujalia tena maisha mapya, ili watu wako wafurahi kwa sababu yako?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Je, hutatuhuisha tena, ili watu wako wakufurahie?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 Je, hutatuhuisha tena, ili watu wako wakufurahie?

Tazama sura Nakili




Zaburi 85:6
15 Marejeleo ya Msalaba  

Nijapopitia katika shida, Unanilinda juu ya hasira ya adui zangu, Unaunyosha mkono wako, Na mkono wako wa kulia unaniokoa.


Israeli na amfurahie Yeye aliyemwumba, Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao.


Laiti wokovu wa Israeli utoke katika Sayuni! MUNGU awarudishapo wafungwa wa watu wake; Yakobo atashangilia, Israeli atafurahi.


Wewe, uliyetuonesha mateso mengi, mabaya, Utatuhuisha tena. Utatupandisha juu tena Kutoka katika vina virefu chini ya nchi.


Ee Mungu, mbona umetutupa milele? Kwa nini hasira yako inatoka moshi Juu ya kondoo wa malisho yako?


Rehema zake zimekoma hata milele? Ahadi yake imekwisha hata vizazi vyote?


Kisha hatutakuacha kwa kurudi nyuma; Utuhuishe nasi tutaliitia jina lako.


Utushibishe asubuhi kwa fadhili zako, Nasi tutashangilia na kufurahi siku zetu zote.


Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.


Je! Ataishika hasira yake hata milele? Ataishika hata mwisho? Tazama, umesema hivyo, bali umetenda mambo mabaya, umefuata njia yako mwenyewe.


itasikika tena sauti ya furaha na sauti ya shangwe, sauti ya bwana arusi na sauti ya bibi arusi, sauti yao wasemao Mshukuruni BWANA wa majeshi, maana BWANA ni mwema, rehema zake ni za milele; na sauti zao waletao sadaka za shukrani nyumbani kwa BWANA. Kwa kuwa nitawarudisha wafungwa wa nchi hii kama kwanza, asema BWANA.


Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua, nasi tutaishi mbele zake.


Ee BWANA, nimesikia habari zako, nami naogopa; Ee BWANA, fufua kazi yako katikati ya miaka; Katikati ya miaka tangaza habari yake; Katika ghadhabu kumbuka rehema.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo