Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 85:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

12 Naam, BWANA atatoa kilicho chema, Na nchi yetu itatoa mazao yake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

12 Naam, Mwenyezi-Mungu atatuletea fanaka, na nchi yetu itatoa mazao yake mengi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

12 Naam, Mwenyezi-Mungu atatuletea fanaka, na nchi yetu itatoa mazao yake mengi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

12 Naam, Mwenyezi-Mungu atatuletea fanaka, na nchi yetu itatoa mazao yake mengi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

12 Naam, hakika Mwenyezi Mungu atatoa kilicho chema, nayo nchi yetu itazaa mavuno yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

12 Naam, hakika bwana atatoa kilicho chema, nayo nchi yetu itazaa mavuno yake.

Tazama sura Nakili




Zaburi 85:12
18 Marejeleo ya Msalaba  

Nchi imetoa mazao yake MUNGU, Mungu wetu, ametubariki.


Na uwepo wingi wa nafaka Katika ardhi juu ya milima; Matunda yake na yawayewaye kama ilivyo katika milima ya Lebanoni, Na watu wa mjini wasitawi kama majani ya nchi.


Kwa kuwa BWANA, Mungu, ni jua na ngao, BWANA atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema Hao waendao kwa ukamilifu.


hata roho itakapomwagwa juu yetu kutoka juu; hata jangwa litakapokuwa shamba lizaalo sana; nalo shamba lizaalo sana litakapohesabiwa kuwa msitu.


Dondokeni, enyi mbingu, toka juu, Mawingu na yamwage haki; Nchi na ifunuke, ili kutoa wokovu, Nayo itoe haki ikamee pamoja; Mimi, BWANA, nimeiumba.


Nayo nchi itazaa matunda yake, nanyi mtakula na kushiba, na kuishi humo salama.


ndipo nitazinyesha mvua zenu kwa nyakati zake, na nchi itazaa mavuno yake, na miti ya mashambani itazaa matunda yake.


Ee mwanadamu, yeye amekuonesha yaliyo mema; na BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!


Kwa maana itakuwako mbegu ya amani; mzabibu utatoa matunda yake, nayo ardhi itatoa mazao yake, na hizo mbingu zitatoa umande wake; nami nitawarithisha mabaki ya watu hawa vitu hivi vyote.


Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kulielewa; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini.


nyingine zikaanguka penye udongo mzuri, zikazaa, moja mia, moja sitini, moja thelathini.


Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapatao elfu tatu.


Nao waliposikia wakamtukuza Mungu, wakamwambia, Ndugu yetu, unaona jinsi Wayahudi walioamini walivyo elfu nyingi, nao wote wana wivu sana kwa ajili ya torati.


Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi;


Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;


Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo