Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 84:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

5 Heri ambaye nguvu zake zatoka kwako, Na njia ziendazo Sayuni zimo moyoni mwake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Heri watu wanaopata nguvu zao kwako, wanaotamani kwenda kuhiji mlimani kwako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Heri watu wanaopata nguvu zao kwako, wanaotamani kwenda kuhiji mlimani kwako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Heri watu wanaopata nguvu zao kwako, wanaotamani kwenda kuhiji mlimani kwako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.

Tazama sura Nakili




Zaburi 84:5
17 Marejeleo ya Msalaba  

Nilifurahi waliponiambia, Twende nyumbani kwa BWANA.


Njoni, enyi watumishi wote wa BWANA, Mhimidini BWANA Ninyi mnaohudumu usiku Katika nyumba ya BWANA.


Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.


Nayakumbuka mambo haya kwa uchungu moyoni mwangu, Jinsi nilivyokuwa nikienda na mkutano, Na kuwaongoza hadi katika nyumba ya Mungu, Kwa sauti ya furaha na kusifu, mkutano wa sikukuu.


Tumehusiana vizuri; na kutembea Nyumbani mwa Mungu pamoja na mkutano.


Kwa mambo ya kutisha utatujibu, Katika haki, Ee Mungu wa wokovu wetu. Wewe uliye tumaini la miisho yote ya dunia, Na la bahari iliyo mbali sana,


Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha, Mshangilieni Mungu wa Yakobo.


Kwa nafsi yangu nimekutamani wakati wa usiku; Naam, kwa nafsi yangu ndani yangu nitakutafuta mapema; Maana hukumu zako zikiwapo duniani, Watu wakaao duniani hujifunza haki.


Mmoja ataniambia, Kwa BWANA, peke yake, iko haki na nguvu; naam, watu watamwendea yeye, na wote waliomkasirikia watatahayarika.


Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema BWANA; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.


Maana kutakuwa siku moja, ambayo walinzi watalia juu ya vilima vya Efraimu, Inukeni, tukaende Sayuni, kwa BWANA, Mungu wetu.


Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njooni, twende juu mlimani kwa BWANA, na nyumbani kwa Mungu wa Yakobo; naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake; kwa maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la BWANA litatoka Yerusalemu.


Nami nitawatia nguvu katika BWANA; nao watatembea huku na huko katika jina lake, asema BWANA.


Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.


Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo