Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 80:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

1 Wewe uchungaye Israeli, usikie, Wewe umwongozaye Yusufu kama kundi; Wewe uketiye juu ya makerubi, utoe nuru.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Utege sikio, ewe Mchungaji wa Israeli, uwaongozaye wazawa wa Yosefu kama kondoo. Ewe ukaaye juu ya viumbe vyenye mabawa, uangaze,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Utege sikio, ewe Mchungaji wa Israeli, uwaongozaye wazawa wa Yosefu kama kondoo. Ewe ukaaye juu ya viumbe vyenye mabawa, uangaze,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Utege sikio, ewe Mchungaji wa Israeli, uwaongozaye wazawa wa Yosefu kama kondoo. Ewe ukaaye juu ya viumbe vyenye mabawa, uangaze,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yusufu kama kundi; wewe uketiye kwenye kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yusufu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza

Tazama sura Nakili




Zaburi 80:1
37 Marejeleo ya Msalaba  

Akaondoka Daudi akaenda pamoja na watu wote waliokuwa naye, mpaka Baala wa Yuda, ili kulipandisha kutoka huko sanduku la Mungu lililoitwa kwa jina, naam, jina la BWANA wa majeshi akaaye juu ya makerubi.


Naye Hezekia akaomba mbele za BWANA, akasema, Ee BWANA, Mungu wa Israeli, ukaaye juu ya makerubi, wewe, naam, wewe peke yako, ndiwe Mungu wa falme zote za dunia; wewe ndiwe uliyeziumba mbingu na nchi.


Je! Ni vema kwako wewe kuonea, Na kuidharau kazi ya mikono yako, Na kuiunga mkono mipango ya waovu?


Moyo wangu umefurika kwa jambo jema, Mimi nasema niliyomfanyia mfalme; Ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi stadi.


Ee BWANA, uyasikilize maneno yangu, Ukuangalie kutafakari kwangu.


Mungu, Mungu BWANA, amenena, ameiita nchi, Toka maawio ya jua hadi machweo yake.


Tokea Sayuni, ukamilifu wa uzuri, Mungu ameangaza kote.


Ee Mungu, uisikilize sala yangu, Wala usijifiche nikuombapo rehema.


Ee Mungu, umetutupa na kututawanya, Umekuwa na hasira, uturudishe tena.


Ee Mungu, uniokoe, Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu.


Uliwaongoza watu wako kama kundi, Kwa mkono wa Musa na Haruni.


Kisha akawaongoza watu wake kama kondoo, Akawachunga kama kundi jangwani.


Ila akaikataa hema ya Yusufu; Wala hakuichagua kabila la Efraimu.


Ee BWANA, Mungu wa majeshi, uturudishe, Uangaze uso wako nasi tutaokoka.


Ee Mungu, uturudishe, Uangaze uso wako nasi tutaokoka.


Ee Mungu wa majeshi, uturudishe, Uangaze uso wako nasi tutaokoka.


Ee BWANA, Mungu wa kisasi, Mungu wa kisasi, uangaze,


BWANA ametamalaki, mataifa wanatetemeka; Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika.


Atalilisha kundi lake kama mchungaji, Atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake; Na kuwachukua kifuani mwake, Nao wanyonyeshao atawaongoza polepole.


Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja, Na utukufu wa BWANA umekuzukia.


Ndipo alipozikumbuka siku za kale, za Musa, na watu wake, akisema, Yuko wapi yeye aliyewapandisha toka baharini pamoja na wachungaji wa kundi lake? Yuko wapi yeye aliyetia kati yao Roho yake Mtakatifu?


Kwa habari za kuonekana kwao wale viumbe hai; kuonekana kwao kulikuwa kama makaa ya moto yawakayo, kama kuonekana kwa vinga vya moto; moto ule ulikuwa ukienda juu na kushuka chini, katikati ya wale viumbe hai; na ule moto ulikuwa na mwangaza mwingi, na katika ule moto ulitoka umeme.


Utukufu wa BWANA ukapaa kutoka kwa kerubi yule, ukasimama juu ya kizingiti cha nyumba; nayo nyumba ikajazwa na lile wingu, na ua ulikuwa umejaa mwangaza wa utukufu wa BWANA.


Nami nitaweka mchungaji mmoja juu yao, naye atawalisha, naam, mtumishi wangu, Daudi; yeye atawalisha, naye atakuwa mchungaji wao.


na tazama, huo utukufu wa Mungu wa Israeli ulitokea kwa njia ya mashariki; na sauti yake ilikuwa kama mshindo wa maji mengi, nayo nchi iling'aa kwa utukufu wake.


Basi sasa, Ee Mungu wetu, yasikilize maombi ya mtumishi wako, na dua zake, ukaangazishe uso wako juu ya patakatifu pako palipo ukiwa, kwa ajili ya Bwana.


Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi;


Akasema, BWANA alitoka Sinai, Akawajia kutoka Seiri; Aliangaza katika kilima cha Parani, Akaja Meribath-kadeshi. Upande wa mkono wake wa kulia Palikuwa na sheria ya motomoto kwao.


Basi, Mungu wa amani aliyemleta tena kutoka kwa wafu Mchungaji Mkuu wa kondoo, kwa damu ya agano la milele, yeye Bwana wetu Yesu,


Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu.


Na Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa, mtalipokea taji la utukufu, lile lisilokauka.


Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-kondoo.


Basi wakatuma watu kwenda Shilo, nao wakalileta toka huko sanduku la Agano la BWANA wa majeshi, akaaye juu ya makerubi; na Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwako huko pamoja na sanduku la Agano la Mungu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo