Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 79:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Ee Mungu wa wokovu wetu, utusaidie, Kwa ajili ya utukufu wa jina lako. Utuokoe, utusamehe dhambi zetu, Kwa ajili ya jina lako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Utusaidie, ee Mungu, mwokozi wetu; kwa heshima ya jina lako utuokoe na kutusamehe dhambi zetu, kwa ajili ya jina lako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Utusaidie, ee Mungu, mwokozi wetu; kwa heshima ya jina lako utuokoe na kutusamehe dhambi zetu, kwa ajili ya jina lako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Utusaidie, ee Mungu, mwokozi wetu; kwa heshima ya jina lako utuokoe na kutusamehe dhambi zetu, kwa ajili ya jina lako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Ee Mungu Mwokozi wetu, utusaidie, kwa ajili ya utukufu wa jina lako; tuokoe na kutusamehe dhambi zetu kwa ajili ya jina lako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Ee Mungu Mwokozi wetu, utusaidie, kwa ajili ya utukufu wa jina lako; tuokoe na kutusamehe dhambi zetu kwa ajili ya jina lako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 79:9
17 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Asa akamlilia BWANA, Mungu wake, akasema, BWANA, hapana kuliko wewe aliye wa kusaidia, kati yake yeye aliye hodari, na yeye asiye na nguvu; utusaidie, Ee BWANA, Mungu wetu; kwa kuwa sisi twakutegemea wewe, na kwa jina lako tumekuja juu ya jamii kubwa hii. Ee BWANA, wewe ndiwe Mungu wetu, asikushinde mwanadamu.


Ee BWANA, kutukuza usitutukuze sisi, Bali ulitukuze jina lako, Kwa ajili ya fadhili zako, Kwa ajili ya uaminifu wako.


Ee BWANA, kwa ajili ya jina lako, Unisamehe uovu wangu, maana ni mwingi.


Ndiwe mwamba wangu na ngome yangu; Kwa ajili ya jina lako uniongoze na unichunge.


Tutakapozidiwa na matendo maovu Wewe utatuondolea uovu wetu.


Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako.


kwa ajili ya jina langu nitaahirisha hasira yangu, na kwa ajili yako nitajizuia, ili nisifiwe, wala nisikukatilie mbali.


Usituchukie, kwa ajili ya jina lako; usikifedheheshe kiti cha enzi cha utukufu wako, kumbuka, usilivunje agano ulilofanya nasi.


Ijapokuwa maovu yetu yanatushuhudia, lakini utende wewe kwa ajili ya jina lako, Ee BWANA, maana kurudi nyuma kwetu ni kwingi; tumekutenda dhambi.


Lakini nilitenda kwa ajili ya jina langu, lisitiwe unajisi machoni pa mataifa, ambao niliwatoa mbele ya macho yao.


Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, nitakapokuwa nimetenda nanyi kwa ajili ya jina langu, si kulingana na njia zenu mbaya, wala si kulingana na matendo yenu maovu, enyi nyumba ya Israeli, asema Bwana MUNGU.


Lakini nilitenda kwa ajili ya jina langu, ili lisitiwe unajisi mbele ya macho ya mataifa, ambao walikaa pamoja nao, ambao machoni pao nilijidhihirisha kwao, kwa kuwatoa katika nchi ya Misri.


Ee Bwana, usikie; Ee Bwana, usamehe; Ee Bwana, usikilize, ukatende, usikawie; kwa ajili yako wewe, Ee Mungu wangu; kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa jina lako.


Rehema na msamaha ni kwa Bwana Mungu wetu, ingawa tumemwasi;


Kama hamtaki kusikia, na kama hamtaki kuitia moyoni, ili kulitukuza jina langu, asema BWANA wa majeshi, basi nitawaleteeni laana, nami nitazilaani baraka zenu; naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamyatii haya moyoni.


Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa.


Maana Wakanaani na wenyeji wote wa nchi hii watasikia habari hii, nao watatuzingira, na kulifuta jina letu katika nchi. Nawe utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo