Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 79:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

5 Ee BWANA, hadi lini? Utaona hasira milele? Wivu wako utawaka kama moto?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Ee Mwenyezi-Mungu, je, utakasirika hata milele? Hasira yako ya wivu itawaka kama moto hata lini?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Ee Mwenyezi-Mungu, je, utakasirika hata milele? Hasira yako ya wivu itawaka kama moto hata lini?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Ee Mwenyezi-Mungu, je, utakasirika hata milele? Hasira yako ya wivu itawaka kama moto hata lini?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Hata lini, Ee Mwenyezi Mungu? Je, wewe utakasirika milele? Wivu wako utawaka kama moto hadi lini?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Hata lini, Ee bwana? Je, wewe utakasirika milele? Wivu wako utawaka kama moto hadi lini?

Tazama sura Nakili




Zaburi 79:5
21 Marejeleo ya Msalaba  

Yeye hatashutumu daima, Wala hatashika hasira yake milele.


BWANA urudi, uniopoe nafsi yangu, Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.


Ee Mungu, mbona umetutupa milele? Kwa nini hasira yako inatoka moshi Juu ya kondoo wa malisho yako?


Ee BWANA, Mungu wa majeshi, hadi lini Utayaghadhibikia maombi ya watu wako?


Umewalisha mkate wa machozi, Umewanywesha machozi kwa kipimo kikuu.


Je! Utatufanyia hasira hata milele? Utadumisha ghadhabu kizazi hadi kizazi?


Hadi lini, Ee BWANA? Utajificha hata milele? Ghadhabu yako itawaka kama moto hadi lini?


Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wa kudumu; Kwa ubatili gani umeiumba jamii ya wanadamu!


Ee BWANA, usione hasira nyingi, wala usiukumbuke uovu siku zote; tazama, angalia, twakusihi, sisi sote tu watu wako.


Ingawa wewe umetukataa kabisa; Nawe una hasira nyingi sana juu yetu.


basi Bwana MUNGU asema hivi; Hakika kwa moto wa wivu wangu nimenena juu ya mabaki ya mataifa, na juu ya Edomu yote, waliojiandalia nchi yangu kuwa milki yao, kwa furaha ya mioyo yao yote, kwa ujeuri wa roho zao, wakatwaa nchi yangu kuwa milki yao, kwa sababu ya malisho yake, ili kuipora;


Ni nani aliye Mungu kama wewe, mwenye kusamehe uovu, na kuliachilia kosa la watu wa urithi wake waliosalia? Hadumishi hasira yake milele, kwa maana yeye hufurahia rehema.


Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya BWANA; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, mwisho wa kutisha.


Basi ningojeeni, asema BWANA, hata siku ile nitakapoondoka kuteka mateka; maana nimeazimia kuwakusanya mataifa, ili nizikutanishe falme, nipate kuwamwagia ghadhabu yangu; naam, ukali wote wa hasira yangu; kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa wivu wangu.


Ndipo yule malaika wa BWANA akajibu, akasema, Ee BWANA wa majeshi, hadi lini utakataa kuurehemu Yerusalemu, na miji ya Yuda uliyoikasirikia miaka hii sabini?


BWANA hatamsamehe mtu huyo, lakini wakati huo hasira ya BWANA na wivu wake vitafuka moshi juu ya mtu yule, na laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki itamkalia juu yake, na BWANA atalifuta jina lake chini ya mbingu.


Wakamtia wivu kwa miungu migeni, Wakamkasirisha kwa machukizo.


Maana, moto umewashwa kwa hasira yangu, Unateketea hata chini ya kuzimu, Unakula dunia pamoja na mazao yake, Unaunguza misingi ya milima.


Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, na Mkweli, utakawia hadi lini kuhukumu na kuilipa damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo