Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 78:69 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

69 Akajenga patakatifu pake kama vilele, Kama dunia aliyoiweka imara milele.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

69 Alijenga hapo hekalu lake kubwa kama mbingu, kama dunia aliyoiweka imara milele.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

69 Alijenga hapo hekalu lake kubwa kama mbingu, kama dunia aliyoiweka imara milele.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

69 Alijenga hapo hekalu lake kubwa kama mbingu, kama dunia aliyoiweka imara milele.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

69 Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.

Tazama sura Nakili




Zaburi 78:69
16 Marejeleo ya Msalaba  

Na ijapokuwa nyumba hii imetukuka namna hii, lakini kila apitaye atashtuka na kuizomea; nao watasema, Kwa nini BWANA ameitenda nchi hii na nyumba hii mambo haya?


Kisha mfalme Daudi akawaambia kusanyiko lote, Sulemani mwanangu, ambaye Mungu amemchagua peke yake, angali ni mchanga bado na hana uzoefu, nayo kazi hii ni kubwa; kwani nyumba hii ya enzi si kwa mwanadamu, ila kwa BWANA, Mungu.


naye Sulemani mwanangu, umjalie ili kwa moyo wote, azishike amri zako, na shuhuda zako, na maagizo yako, akayatende hayo yote na kuijenga nyumba hii ya enzi, niliyoiwekea akiba.


ili wanitengenezee miti kwa wingi; kwani nyumba nitakayoijenga itakuwa kubwa ajabu.


Na ukumbi uliokuwa mbele yake, urefu wake ulikuwa sawa na upana wa nyumba ulikuwa dhiraa ishirini, na kimo chake mia moja na ishirini; akaufunikiza ndani kwa dhahabu safi.


Yeye hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu, Na kuutundika ulimwengu pasipo kitu.


Hapo mwanzo uliutia msingi wa nchi, Na mbingu ni kazi ya mikono yako.


Uliiweka nchi juu ya misingi yake, Isitikisike milele.


Msingi wake upo Juu ya milima mitakatifu.


Naam, mkono wangu umeuweka msingi wa dunia, na mkono wangu wa kulia umezitanda mbingu; niziitapo husimama pamoja.


Inueni macho yenu mbinguni, mkaitazame nchi chini; maana mbingu zitatoweka kama moshi, na nchi itachakaa kama vazi, nao wakaao ndani yake watakufa kadhalika; bali wokovu wangu utakuwa wa milele, na ukombozi wangu hautakoma kamwe.


Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.


Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Humpandisha mhitaji kutoka jaani, Ili awaketishe pamoja na wakuu, Wakakirithi kiti cha enzi cha utukufu; Kwa maana nguzo za dunia zina BWANA, Naye ameuweka ulimwengu juu yake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo