Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 77:14 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

14 Wewe ndiwe Mungu ufanyaye maajabu; Uliudhihirisha uweza wako kati ya mataifa.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

14 Wewe ni Mungu unayetenda maajabu; wewe umeyaonesha mataifa uwezo wako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

14 Wewe ni Mungu unayetenda maajabu; wewe umeyaonesha mataifa uwezo wako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

14 Wewe ni Mungu unayetenda maajabu; wewe umeyaonesha mataifa uwezo wako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

14 Wewe ndiwe Mungu utendaye miujiza, umeonesha uwezo wako kati ya mataifa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

14 Wewe ndiwe Mungu utendaye miujiza, umeonyesha uwezo wako katikati ya mataifa.

Tazama sura Nakili




Zaburi 77:14
15 Marejeleo ya Msalaba  

Yakumbukeni matendo yake ya ajabu aliyoyafanya, Miujiza yake na hukumu alizotoa.


Lakini akawaokoa kwa ajili ya jina lake, Ayadhihirishe matendo yake makuu.


Yeye peke yake afanya maajabu makuu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.


Waimbaji hutangulia, nyuma yao wapigao vinanda, Kati ya wanawali wapiga matari.


Na ahimidiwe BWANA, Mungu, Mungu wa Israeli, Atendaye miujiza Yeye peke yake;


Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu, Wewe ndiwe mfanya miujiza, Ndiwe Mungu peke yako.


Kisha itakuwa hapo mwanao atakapokuuliza kesho, akisema, Ni nini hivi? Utamwambia, BWANA alimtoa Misri, kutoka ile nyumba ya utumwa, kwa uwezo wa mkono wake;


Ee BWANA, katika miungu ni nani aliye kama wewe? Ni nani aliye kama wewe, mtukufu katika utakatifu, Mwenye kuogopwa katika sifa zako, mfanya maajabu?


BWANA, mkono wako wa kulia umepata fahari ya uwezo, BWANA, mkono wako wa kulia wawasetaseta adui.


Amka, amka, jivike nguvu, Ee mkono wa Bwana; Amka kama katika siku zile za kale, Katika vizazi vile vya zamani.


BWANA ameweka wazi mkono wake mtakatifu Machoni pa mataifa yote; Na ncha zote za dunia Zitauona wokovu wa Mungu wetu.


Basi mimi naweka amri ya kuwa kila kabila la watu, na kila taifa, na kila lugha, watakaonena neno lolote lisilopasa juu ya huyo Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego, watakatwa vipande vipande, na nyumba zao zitafanywa jaa; kwa kuwa hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.


Yeye huponya na kuokoa, hutenda ishara na maajabu mbinguni na duniani, ndiye aliyemponya Danieli na nguvu za simba.


Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo