Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 74:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

1 Ee Mungu, mbona umetutupa milele? Kwa nini hasira yako inatoka moshi Juu ya kondoo wa malisho yako?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Kwa nini, ee Mungu, umetutupa kabisa? Mbona hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wako!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Kwa nini, ee Mungu, umetutupa kabisa? Mbona hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wako!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Kwa nini, ee Mungu, umetutupa kabisa? Mbona hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wako!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Ee Mungu, mbona umetukataa milele? Mbona hasira yako inatoka moshi juu ya kondoo wa malisho yako?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Ee Mungu, mbona umetukataa milele? Mbona hasira yako inatoka moshi juu ya kondoo wa malisho yako?

Tazama sura Nakili




Zaburi 74:1
30 Marejeleo ya Msalaba  

Nami nitawatupa mabaki ya urithi wangu, na kuwatia mikononi mwa adui zao; nao watakuwa nyara na mateka kwa adui zao wote;


Ee BWANA, kwa nini wasimama mbali? Kwani unajificha nyakati za shida?


Jueni kwamba BWANA ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.


Kukapanda moshi kutoka puani mwake, Moto wa kuteketeza ukatoka kinywani mwake, Makaa ya moto yakamtoka.


Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.


Nitamwambia Mungu, mwamba wangu, Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?


Lakini umetutupa, umetufedhehesha, Wala huendi na majeshi yetu.


Mungu, Mungu BWANA, amenena, ameiita nchi, Toka maawio ya jua hadi machweo yake.


Ee Mungu, umetutupa na kututawanya, Umekuwa na hasira, uturudishe tena.


Ee Mungu, si Wewe uliyetutupa? Wala, Ee Mungu, hutoki na majeshi yetu?


Je! Bwana atatutupa milele na milele? Asiwe na fadhili kwetu kamwe?


Rehema zake zimekoma hata milele? Ahadi yake imekwisha hata vizazi vyote?


Enyi watu wangu, sikilizeni sheria yangu, Tegeni masikio kwa maneno ya kinywa changu.


Na sisi tulio watu wako, Na kondoo za malisho yako, Tutakushukuru milele; Tutazisimulia sifa zako kizazi hadi kizazi.


Ee BWANA, hadi lini? Utaona hasira milele? Wivu wako utawaka kama moto?


Umewalisha mkate wa machozi, Umewanywesha machozi kwa kipimo kikuu.


Je! Hutaki kurudi na kutuhuisha, Ili watu wako wakufurahie?


Kwa maana ndiye Mungu wetu, Na sisi tu watu wa malisho yake, Na kondoo za mkono wake. Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!


Musa akamsihi sana BWANA, Mungu wake, na kusema, BWANA, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?


Lakini sasa, Ee BWANA, wewe u baba yetu; sisi tu udongo, nawe u mfinyanzi wetu; sisi sote tu kazi ya mikono yako.


Ole wao wachungaji, wanaoharibu kondoo za malisho yangu na kuwatawanya! Asema BWANA.


BWANA asema hivi, Kama mbingu zikiweza kupimwa, na misingi ya dunia ikiweza kugunduliwa huko chini, ndipo wazao wa Israeli pia nitawatupilia mbali, kwa ajili ya hayo yote waliyoyatenda, asema BWANA.


Ingawa wewe umetukataa kabisa; Nawe una hasira nyingi sana juu yetu.


Na ninyi, kondoo wangu, kondoo wa malisho yangu, ni wanadamu, na mimi ni Mungu wenu, asema Bwana MUNGU.


Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, kwa sababu kondoo wangu walikuwa mateka, kondoo wangu wakawa chakula cha wanyamamwitu wote, kwa sababu hapakuwa na mchungaji, wala wachungaji wangu hawakutafuta kondoo wangu, bali wachungaji walijilisha wenyewe wala hawakuwalisha kondoo wangu;


Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.


BWANA hatamsamehe mtu huyo, lakini wakati huo hasira ya BWANA na wivu wake vitafuka moshi juu ya mtu yule, na laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki itamkalia juu yake, na BWANA atalifuta jina lake chini ya mbingu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo