Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 73:27 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

27 Maana wajitengao nawe watapotea; Umewaangamiza wote waliokuacha Wewe.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

27 Anayejitenga nawe, hakika ataangamia. Anayekukana, utamwangamiza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

27 Anayejitenga nawe, hakika ataangamia. Anayekukana, utamwangamiza.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

27 Anayejitenga nawe, hakika ataangamia. Anayekukana, utamwangamiza.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

27 Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 73:27
15 Marejeleo ya Msalaba  

Basi Sauli alikufa kwa sababu ya kosa lake alilomkosa BWANA, kwa sababu ya neno la BWANA, asilolishika; na tena kwa kutaka shauri kwa mwenye pepo wa utambuzi, aulize kwake,


Akapeleka barua kwa Wayahudi wote katika majimbo yote mia moja ishirini na saba ya ufalme wake Ahasuero, maneno ya amani na kweli,


Ndivyo walivyotiwa uchafu kwa kazi zao, Wakafanya uasherati kwa matendo yao.


Wokovu u mbali na wasio haki, Kwa maana hawajifunzi amri zako.


Usije ukafanya agano na wenyeji wa nchi, watu wakaenda kufanya uzinzi na miungu yao, na kuitolea sadaka miungu yao; mtu mmoja akakuita, ukaila sadaka yake.


Bwana akanena, Kwa kuwa watu hawa hunikaribia na kuniheshimu kwa vinywa vyao, bali mioyo yao wamefarakana nami, na kicho chao walichonacho kwangu ni maagizo ya wanadamu waliyofundishwa;


Umewapanda, naam, wametia mizizi, wanakua, naam, wanazaa matunda; katika vinywa vyao u karibu, bali katika mioyo yao u mbali.


Ee BWANA, tumaini la Israeli, wote wakuachao watatahayarika. Wao watakaojitenga nami wataandikwa katika mchanga, kwa sababu wamemwacha BWANA, kisima cha maji yaliyo hai.


nacho kitakuwa kwenu ni kishada, ili mpate kukiangalia, na kuyakumbuka maagizo yote ya BWANA, na kuyafanya; tena ili msiende kutangatanga kufuata mioyo yenu wenyewe, na macho yenu wenyewe, ambayo mlikuwa mkiyaandama kwa uasherati hapo kwanza;


Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo.


Akaja akahubiri amani kwenu ninyi mliokuwa mbali, na amani kwao wale waliokuwa karibu.


Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo