Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 73:24 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

24 Utaniongoza kwa shauri lako, Na baadaye utanikaribisha kwa utukufu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

24 Wewe waniongoza kwa mashauri yako; mwishowe utanipokea kwenye utukufu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

24 Wewe waniongoza kwa mashauri yako; mwishowe utanipokea kwenye utukufu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

24 Wewe waniongoza kwa mashauri yako; mwishowe utanipokea kwenye utukufu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

24 Unaniongoza kwa ushauri wako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

24 Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.

Tazama sura Nakili




Zaburi 73:24
25 Marejeleo ya Msalaba  

Nitamhimidi BWANA aniongozaye, Wakati wa usiku pia moyo wangu hunishauri.


Wenye upole atawaongoza katika haki, Wenye upole atawafundisha njia yake.


Nitakufundisha na kukuonesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.


Kwa maana ndivyo alivyo MUNGU, Mungu wetu. Milele na milele Yeye ndiye atakayetuongoza.


Bali Mungu atanikomboa nafsi yangu, Atanitoa mkononi mwa kuzimu, maana atanipokea.


Kwa kuwa BWANA, Mungu, ni jua na ngao, BWANA atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema Hao waendao kwa ukamilifu.


Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu.


na masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.


BWANA, mkombozi wako, mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.


Naye BWANA atakuongoza daima, ataishibisha nafsi yako mahali pasipokuwa na maji, na kuitia nguvu mifupa yako; nawe utakuwa kama bustani iliyotiwa maji, na kama chemchemi ambayo maji yake hayapungui.


Ndipo nuru yako itakapopambazuka kama asubuhi, na uponyaji wako utatokea punde; na haki yako itakutangulia; utukufu wa BWANA utakufuata nyuma ukulinde.


Ikiwa lile wingu lilikawia, likikaa juu ya maskani siku mbili, au mwezi, au mwaka, wana wa Israeli walikaa katika kambi yao, wasisafiri;


Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?


Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.


Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi muwepo.


Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.


Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami popote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu.


Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.


Wakampiga kwa mawe Stefano, naye akiomba, akisema, Bwana Yesu, pokea roho yangu.


Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni.


Wala wasiwe na urithi kati ya ndugu zao; BWANA ndiye urithi wao, kama alivyowaambia.


Lakini mmoja wenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo