Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 73:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, Kwa hao walio safi mioyo yao.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Hakika, Mungu ni mwema kwa watu wanyofu; ni mwema kwa walio safi moyoni.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Hakika, Mungu ni mwema kwa watu wanyofu; ni mwema kwa walio safi moyoni.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Hakika, Mungu ni mwema kwa watu wanyofu; ni mwema kwa walio safi moyoni.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.

Tazama sura Nakili




Zaburi 73:1
24 Marejeleo ya Msalaba  

Basi Walawi wakamwagiza Hemani mwana wa Yoeli; na wa nduguze, Asafu mwana wa Berekia; na wa wana wa Merari ndugu zao, Ethani mwana wa Kishi;


Basi akawaacha huko, mbele ya sanduku la Agano la BWANA, Asafu na nduguze, ili watumike mbele ya sanduku daima, kila siku kama ilivyokuwa kazi yake.


Ndipo siku hiyo Daudi alipoagiza kwanza kumshukuru BWANA, kwa mkono wa Asafu na nduguze.


Na nduguye Asafu, aliyesimama upande wake wa kulia, huyo Asafu alikuwa mwana wa Berekia, mwana wa Shimea;


Tena Hezekia mfalme na wakuu wakawaamuru Walawi, wamwimbie BWANA sifa kwa maneno ya Daudi, na ya Asafu mwonaji. Wakaimba sifa kwa furaha, wakainamisha vichwa, wakaabudu.


Nami nimemweka mfalme wangu Juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.


Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiweka nafsi yake katika uongo, Wala hakuapa kwa hila.


Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.


Mungu, Mungu BWANA, amenena, ameiita nchi, Toka maawio ya jua hadi machweo yake.


Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya na kuithibiti roho yangu.


Hakika Wewe huwaweka penye utelezi, Huwaangusha mpaka palipoharibika.


Ee Mungu, usistarehe, Ee Mungu, usinyamae, wala usitulie.


Kwa kuwa BWANA, Mungu, ni jua na ngao, BWANA atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema Hao waendao kwa ukamilifu.


Ee Yerusalemu, jioshe moyo wako usiwe na uovu, upate kuokoka. Mawazo yako mabaya yatakaa ndani yako hata lini?


Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu.


Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.


Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake.


Kwa hiyo ilitoka katika imani, iwe kwa njia ya neema, ili kwamba ile ahadi iwe imara kwa wazawa wote; si kwa wale wa torati tu, ila na kwa wale wa imani ya Abrahamu; aliye baba yetu sisi sote;


si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa mara ya pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu;


Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo