Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 72:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

5 Watakuogopa wakati wote wa kudumu jua, Na wakati wa kung'aa mwezi kizazi hata kizazi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Mfalme aishi muda mrefu kama jua, na kama mwezi, kwa vizazi vyote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Mfalme aishi muda mrefu kama jua, na kama mwezi, kwa vizazi vyote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Mfalme aishi muda mrefu kama jua, na kama mwezi, kwa vizazi vyote.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Atadumu kama jua linavyodumu, kama mwezi, vizazi vyote.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.

Tazama sura Nakili




Zaburi 72:5
14 Marejeleo ya Msalaba  

Na Israeli wote wakapata habari za hukumu ile aliyoihukumu mfalme wakamwogopa mfalme; maana waliona ya kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake, ili afanye hukumu.


Jina lake na lidumu milele, Pindi ling'aapo jua, umaarufu wake uwepo; Mataifa yote na wabarikiwe katika yeye, Na kumwita heri.


Haki na isitawi wakati wa maisha yake yote, Nayo amani iwepo, hadi mwezi utakapokoma.


Wazao wake nao nitawadumisha milele, Na kiti chake cha enzi kama siku za mbingu.


Mamlaka ya enzi yake yatakuzwa daima, Na kutakuwa na amani isiyo na mwisho, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa BWANA wa majeshi ndio utakaotenda hayo.


Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.


Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.


Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye Juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii.


naam, atukuzwe katika kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina.


Malaika wa saba akapiga baragumu, pakawa na sauti kuu katika mbingu, zikisema, Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atamiliki hata milele na milele.


Basi Samweli akamwomba BWANA, naye BWANA akatuma ngurumo na mvua siku ile; nao watu wote wakamwogopa BWANA sana, na Samweli pia.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo