Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 72:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

2 Atawaamua watu wako kwa haki, Na watu wako walioonewa kwa hukumu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 atawale taifa lako kwa haki, na maskini wako kwa uadilifu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 atawale taifa lako kwa haki, na maskini wako kwa uadilifu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 atawale taifa lako kwa haki, na maskini wako kwa uadilifu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.

Tazama sura Nakili




Zaburi 72:2
18 Marejeleo ya Msalaba  

Mungu wa Israeli alisema, Mwamba wa Israeli aliniambia, Atawalaye wanadamu kwa haki, Akitawala katika kicho cha Mungu,


Na ahimidiwe BWANA, Mungu wako, aliyependezwa nawe, ili akuweke juu ya kiti cha enzi cha Israeli; kwa kuwa BWANA amewapenda Israeli milele, kwa hiyo amekufanya kuwa mfalme, ufanye hukumu na haki.


Na Israeli wote wakapata habari za hukumu ile aliyoihukumu mfalme wakamwogopa mfalme; maana waliona ya kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake, ili afanye hukumu.


naye Sulemani mwanangu, umjalie ili kwa moyo wote, azishike amri zako, na shuhuda zako, na maagizo yako, akayatende hayo yote na kuijenga nyumba hii ya enzi, niliyoiwekea akiba.


Sembuse yeye huwajali nyuso za wakuu, Wala hawajali matajiri kuliko maskini? Kwani wote ni kazi ya mikono yake,


Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge, Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji, Sasa nitasimama, asema BWANA, Nitamweka salama yeye wanayemfyonya.


Mfalme awahukumuye maskini kwa uaminifu; Kiti chake cha enzi kitathibitika milele.


Tazama, mfalme atamiliki kwa haki, na wakuu watatawala kwa hukumu.


Na kazi ya haki itakuwa amani; na mazao ya haki yatakuwa ni utulivu na matumaini daima.


Mamlaka ya enzi yake yatakuzwa daima, Na kutakuwa na amani isiyo na mwisho, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa BWANA wa majeshi ndio utakaotenda hayo.


Katika siku zile, na wakati ule, nitamchipushia Daudi Chipukizi la haki; naye atafanya hukumu na haki katika nchi hii.


Nami nitawatafuta waliopotea, nitawarudisha waliotangatanga, nitawatibu waliojeruhiwa, nitawatia nguvu wagonjwa; nao wanono na wenye nguvu nitawaharibu; nitawalisha hukumu.


Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo