Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 71:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Usinitupe wakati wa uzee, Nguvu zangu zipungukapo usiniache.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Wakati wa uzee usinitupe; niishiwapo na nguvu usiniache.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Wakati wa uzee usinitupe; niishiwapo na nguvu usiniache.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Wakati wa uzee usinitupe; niishiwapo na nguvu usiniache.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.

Tazama sura Nakili




Zaburi 71:9
10 Marejeleo ya Msalaba  

Sasa nina miaka themanini; nami je! Naweza kupambanua mema na mabaya? Mimi mtumishi wako, je! Naweza kuonja nilacho au ninywacho? Naweza kusikia tena sauti ya waimbaji wa kiume na wa kike? Kwa nini basi mtumishi wako azidi kumlemea bwana wangu mfalme?


Na hata nikiwa ni mzee mwenye mvi, Ee Mungu, usiniache. Hata niwaeleze watu wa kizazi hiki nguvu zako, Na kila atakayekuja uweza wako.


Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele.


Miaka ya maisha yetu ni sabini, Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini; Tena kiburi chake ni taabu na ubatili, Maana wakati unapita upesi nasi kutokomea punde.


na hata uzee wenu mimi ndiye, na hata wakati wenu wa mvi nitawachukueni; nimefanya, nami nitachukua; naam, nitachukua na kuokoa.


Kwa sababu hiyo nimepatikana na mateso haya, lakini sitahayari; kwa maana namjua yeye niliyemwamini, na kusadiki ya kwamba aweza kukilinda kile nilichokiweka amana kwake hata siku ile.


Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike katika ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo