Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 65:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

2 Wewe usikiaye maombi, Wote wenye mwili watakujia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 maana wewe wajibu sala zetu. Binadamu wote watakujia wewe.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 maana wewe wajibu sala zetu. Binadamu wote watakujia wewe.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 maana wewe wajibu sala zetu. Binadamu wote watakujia wewe.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 Ewe usikiaye maombi, watu wote watakuja kwako wewe.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 Ewe usikiaye maombi, kwako wewe watu wote watakuja.

Tazama sura Nakili




Zaburi 65:2
23 Marejeleo ya Msalaba  

Ikawa, wakati wa adhuhuri ulipopita, walitabiri hata wakati wa kutoa dhabihu ya jioni; lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu, wala aliyeangalia.


Unisikie, Ee BWANA, unisikie, ili watu hawa wajue ya kuwa wewe, BWANA, ndiwe Mungu, na ya kuwa wewe umewageuza moyo wakurudie.


Akamwomba; naye akamtakabali, akayasikia maombi yake; akamrudisha tena Yerusalemu katika ufalme wake. Ndipo Manase akajua ya kwamba BWANA ndiye Mungu.


Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, Asiyadharau maombi yao.


Nitaziondoa nadhiri zangu kwa BWANA, Naam, mbele ya watu wake wote.


Nitaziondoa nadhiri zangu kwa BWANA, Naam, mbele ya watu wake wote.


Miisho yote ya dunia itakumbuka, Na watu watamrejea BWANA; Jamaa zote za mataifa watamsujudia.


Nitaingia nyumbani mwako na kafara; Nitaondoa kwako nadhiri zangu;


Hakika Mungu amesikia; Ameisikiliza sauti ya maombi yangu.


Nchi yote itakusujudia na kukuimbia, Naam, italiimbia jina lako.


Mataifa yote uliyoyaumba watakuja; Watakusujudia Wewe, Bwana, Watalitukuza jina lako;


naam, asema hivi, Ni neno dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kuyainua makabila ya Yakobo, na kuwarejesha watu wa Israeli waliohifadhiwa; zaidi ya hayo nitakutoa uwe nuru ya mataifa, upate kuwa wokovu wangu hata miisho ya dunia.


Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa bado wanena, nitasikia.


Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema BWANA.


Yeye apondaye vipande vipande amepanda juu mbele ya uso wako; zishike silaha, ilinde njia, vitie nguvu viuno vyako, uongeze uwezo wako sana.


Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu.


akasema, Kornelio, kuomba kwako kumesikiwa, na sadaka zako zinakumbukwa mbele za Mungu.


Malaika wa saba akapiga baragumu, pakawa na sauti kuu katika mbingu, zikisema, Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atamiliki hata milele na milele.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo