Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 59:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe, Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Nitakungoja, ewe uliye nguvu yangu; maana wewe, ee Mungu, u ngome yangu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Nitakungoja, ewe uliye nguvu yangu; maana wewe, ee Mungu, u ngome yangu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Nitakungoja, ewe uliye nguvu yangu; maana wewe, ee Mungu, u ngome yangu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,

Tazama sura Nakili




Zaburi 59:9
18 Marejeleo ya Msalaba  

Yeye aketiye mbinguni anacheka, Bwana anawafanyia dhihaka.


BWANA akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.


BWANA ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? BWANA ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?


Umtumainie BWANA, uwe imara, Upige moyo konde, naam, umngoje BWANA.


Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.


BWANA wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.


Ee nguvu zangu, nitakuimbia sifa, Maana Ewe Mungu ndiwe ngome yangu, Mungu wa fadhili zangu.


Mara moja amenena Mungu; Mara mbili nimeyasikia haya, Ya kuwa nguvu zina Mungu,


Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika.


BWANA atakuwa ngome kwake aliyeonewa, Naam, ngome kwa nyakati za shida.


Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; Nitatumaini wala sitaogopa; Maana BWANA YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu.


bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watakimbia, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.


ndipo utakapojifurahisha katika BWANA; nami nitakupandisha mahali pa nchi palipoinuka; nitakulisha urithi wa Yakobo baba yako; kwa maana kinywa cha BWANA kimenena hayo.


MUNGU, aliye BWANA, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka.


Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]


Tufuate:

Matangazo


Matangazo