Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 56:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

7 Je! Wataokoka kwa uovu wao? Ee Mungu, uwaangamize kwa hasira yako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Ee Mungu, uwalipe kwa kadiri ya uovu wao, uwaangushe hao waovu kwa hasira yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Ee Mungu, uwalipe kwa kadiri ya uovu wao, uwaangushe hao waovu kwa hasira yako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Ee Mungu, uwalipe kwa kadiri ya uovu wao, uwaangushe hao waovu kwa hasira yako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.

Tazama sura Nakili




Zaburi 56:7
14 Marejeleo ya Msalaba  

Huko ndiko walikoanguka wafanyao maovu; Wameangushwa chini wasiweze kusimama.


Mtu asiye haki humvizia mwenye haki, Na kutafuta jinsi ya kumwua.


Ambao wanazitumainia mali zao, Na kujisifia wingi wa utajiri wao;


Mauti na iwapate kwa ghafla, Na washuke kuzimu wangali hai, Maana uovu uko nyumbani mwao moyoni mwao.


Nawe, Ee Mungu, utawateremsha, Wafikie shimo la uharibifu; Watu wa damu na hila hawataishi nusu ya siku zao, Bali mimi nitakutumaini Wewe.


Ee Bwana, uwaangamize, uzivuruge ndimi zao, Maana nimeona dhuluma na fitina katika mji.


Bila kosa langu wanaenda mbio, kujiweka tayari; Inuka utazame na kunisaidia.


Hakuna mwenye uwezo juu ya roho aizuie roho; Wala hana mamlaka juu ya siku ya kufa; Wala hakuna kuponyoka katika vita vile; Wala uovu hautamwokoa yule aliyeuzoea.


Kwa sababu mmesema, Tumefanya agano na mauti, tumepatana na kuzimu; pigo lifurikalo litakapopita, halitatufikia sisi; kwa maana tumefanya maneno ya uongo kuwa kimbilio letu, tumejificha chini ya maneno yasiyo kweli;


Hasira yako uwamwagie mataifa wasiokujua, na jamaa zao wasioliitia jina lako; kwa maana wamemla Yakobo, naam, wamemla kabisa na kumwangamiza, na kuyafanya makao yake kuwa ukiwa.


kisha mtakuja na kusimama mbele zangu katika nyumba hii, iitwayo kwa jina langu, na kusema, Tumepona; ili mpate kufanya machukizo hayo yote?


Wewe uliye na macho safi hata usiweze kuangalia uovu, wewe usiyeweza kutazama ukaidi, mbona unawaangalia watendao kwa hila; na kunyamaza kimya, hapo mtu mwovu ammezapo mtu aliye mwenye haki kuliko yeye;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo