Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 56:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

1 Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, Mchana kutwa ananionea akileta vita.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Ee Mungu, unionee huruma, maana watu wananishambulia. Mchana kutwa maadui wananidhulumu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Ee Mungu, unionee huruma, maana watu wananishambulia. Mchana kutwa maadui wananidhulumu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Ee Mungu, unionee huruma, maana watu wananishambulia. Mchana kutwa maadui wananidhulumu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.

Tazama sura Nakili




Zaburi 56:1
25 Marejeleo ya Msalaba  

Nchi ikapasuka ikammeza Dathani, Ikaufunika mkutano wa Abiramu.


Papo hapo wangalitumeza hai, Hasira yao ilipowaka juu yetu.


Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wao wa kwanza; Kwa maana fadhili zake ni za milele.


Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.


Kwa fadhili zako utawakatilia mbali adui zangu; Na kuwaangamiza wote wanitesao nafsi, Kwa maana mimi ni mtumishi wako.


Mungu, unihifadhi mimi, Kwa maana nakukimbilia Wewe.


Utawafanya kuwa kama tanuri ya moto, Wakati wa ghadhabu yako. BWANA atawameza kwa ghadhabu yake, Na moto utawateketeza.


Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka.


Ee BWANA, unifadhili, maana ni katika dhiki, Jicho langu limenyauka kwa masumbufu, Naam, mwili wangu na nafsi yangu.


Wasiseme moyoni, Haya! Ndivyo tutakavyo; Wasiseme, Tumemmeza.


Ni kweli, enyi wakuu, mnanena haki? Enyi wanadamu, mnahukumu kwa adili?


Ee Mungu wangu, uniponye na adui zangu, Uniinue juu yao wanaoshindana nami.


Mungu wa fadhili zangu atanitangulia, Mungu atanijalia kutazama kwa ushindi juu ya adui zangu.


Ee Mungu, umetutupa na kututawanya, Umekuwa na hasira, uturudishe tena.


Tuwameze hai kama kuzimu, Na wazima, kama wao washukao shimoni.


Juu yako adui zako wote Wamepanua vinywa vyao; Huzomea, husaga meno yao, Husema, Tumemmeza; Hakika siku hii ndiyo tuliyoitazamia; Tumeipata, tumeiona.


Bwana ameyameza makao yote ya Yakobo, Wala hakuona huruma; Ameziangusha ngome za binti Yuda Katika ghadhabu yake; Amezibomoa hata nchi Ameunajisi ufalme na wakuu wake.


Bwana amekuwa mfano wa adui, Amemmeza Israeli; Ameyameza majumba yake yote, Ameziharibu ngome zake; Tena amemzidishia binti Yuda Matanga na maombolezo.


Israeli amemezwa; sasa wamo miongoni mwa mataifa kama chombo kisichopendeza.


Basi huu uharibikao utakapovaa kutoharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa katika ushindi.


Lakini wakuu wa Wafilisti wakamkasirikia, na kumwambia, Mrudishe huyu, apate kurejea mahali pake ulipomwagiza, wala asiende pamoja nasi vitani, asije akawa adui wetu vitani; kwani mtu huyu angejipatanisha na bwana wake kwa njia gani? Je! Si kwa vichwa vya watu hawa?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo