Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 55:20 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

20 Mwenzangu amenyosha mkono awadhuru waliopatana naye, Amelivunja agano lake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

20 Mwenzangu amewashambulia rafiki yake, amevunja mapatano yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

20 Mwenzangu amewashambulia rafiki yake, amevunja mapatano yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

20 Mwenzangu amewashambulia rafiki yake, amevunja mapatano yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

20 Mwenzangu hushambulia rafiki zake, naye huvunja agano lake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

20 Mwenzangu hushambulia rafiki zake, naye huvunja agano lake.

Tazama sura Nakili




Zaburi 55:20
20 Marejeleo ya Msalaba  

Yule mtu akamwambia Yoabu, Kama ningalipata fedha elfu moja mkononi mwangu, hata hivyo singalinyosha mkono wangu juu ya mwana wa mfalme; kwa maana mfalme masikioni mwetu alikuagiza wewe, na Abishai na Itai, akisema, Angalieni sana mtu yeyote yule asimguse yule kijana, Absalomu.


Basi watu wa Yuda wakaenda, wakamtia Daudi mafuta huko, awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Wakamwambia Daudi wakasema, Watu wa Yabesh-gileadi ndio waliomzika Sauli.


Basi wazee wote wa Israeli wakamwendea mfalme huko Hebroni, naye mfalme Daudi akapatana nao huko Hebroni mbele za BWANA; wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya Israeli.


Hata siku hii ya leo hufanya sawasawa na kawaida za kwanza; wala hawamwogopi BWANA, wala hawazifuati sheria zao, wala hukumu zao, wala ile torati, wala ile amri BWANA aliyowaamuru wana wa Yakobo, ambaye alimpa jina la Israeli;


Wamenilipa mabaya kwa mema yangu, Na chuki badala ya upendo wangu.


Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, Watarudi nyuma, kwa ghafla wataaibika.


Ikiwa nimemlipa mabaya Yeye aliyekaa kwangu salama; (Hasha! Nimemponya yeye Aliyekuwa mtesi wangu bila sababu;)


Hata milele nitamwekea fadhili zangu, Na agano langu naye litadumu hata milele.


Mimi sitalivunja agano langu, Sitalibadili neno lililotoka midomoni mwangu.


Lakini wewe umemtupa na kumkataa, Umemghadhibikia masihi wako.


Kiti chako kimekuwa thabiti tokea zamani; Wewe ndiwe uliye tangu milele.


Mimi nasema hivi, Uishike amri ya mfalme; na hiyo kwa sababu umeapa kwa Mungu.


Ee BWANA, macho yako je! Hayaangalii uaminifu? Umewapiga, lakini hawakuhuzunika; umewakomesha, lakini wamekataa kurudiwa wamefanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko mwamba wamekataa kurudi.


Karibu wakati ule ule, Herode mfalme akanyosha mikono yake kuwatenda mabaya baadhi ya watu wa kanisa.


Kisha mfalme akawaambia askari walinzi waliosimama karibu naye Geukeni, mkawaue hao makuhani wa BWANA, kwa sababu mkono wao u pamoja na Daudi, na kwa sababu walijua ya kuwa amekimbia, wasiniarifu. Lakini watumishi wa mfalme walikataa kunyosha mkono na kuwaangukia makuhani wa BWANA.


Tazama, leo hivi macho yako yameona jinsi BWANA alivyokutia mikononi mwangu pangoni, na watu wengine wakaniambia nikuue; lakini nikakuacha; nikasema, Sitaki kuunyosha mkono wangu juu ya bwana wangu; kwa maana yeye ni masihi wa BWANA.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo