Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 46:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

3 Maji yake yajapovuma na kuumuka, Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 hata kama bahari ikichafuka na kutisha, na milima ikatetemeka kwa machafuko yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 hata kama bahari ikichafuka na kutisha, na milima ikatetemeka kwa machafuko yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 hata kama bahari ikichafuka na kutisha, na milima ikatetemeka kwa machafuko yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 hata maji yake yakinguruma na kuumuka, na milima itetemeke kwa mawimbi yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.

Tazama sura Nakili




Zaburi 46:3
17 Marejeleo ya Msalaba  

Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za BWANA. Na tazama, BWANA akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunjavunja miamba mbele za BWANA; lakini BWANA hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini BWANA hakuwamo katika lile tetemeko la nchi;


Nikasema, Utafika mpaka hapa, lakini hutapita, Na hapa mawimbi yako yenye nguvu yatazuiliwa?


Kamba za mauti zilinizunguka, Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.


Na sasa, enyi wenyeji wa Yerusalemu, nanyi watu wa Yuda, amueni, nawasihi, kati ya mimi na shamba langu la mizabibu.


Maana milima itaondoka, na vilima vitaondolewa; bali wema wangu hautaondoka kwako, wala agano langu la amani halitaondolewa; asema BWANA akurehemuye.


Niliiangalia milima, na tazama, ilitetemeka, na milima yote ilisogea huku na huko.


Je! Hamniogopi mimi? Asema BWANA; hamtatetemeka mbele za uso wangu; mimi niliyeweka mchanga kuwa mpaka wa bahari, kwa amri ya daima, isiweze kuupita? Mawimbi yake yajapoumuka-umuka, hayawezi kushinda nguvu; yajapovuma sana, hayawezi kuupita.


Na hiyo milima itayeyuka chini yake, nayo mabonde yatapasuliwa, kama vile nta iliyo mbele ya moto, kama maji yaliyomwagika katika mteremko.


Milima hutetema mbele zake, navyo vilima huyeyuka; nayo dunia huinuliwa mbele za uso wake, naam, dunia na wote wakaao ndani yake.


mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.


Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.


Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo