Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 43:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

2 Kwa kuwa Wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 Nakimbilia usalama kwako ee Mungu; kwa nini umenitupilia mbali? Yanini niende huko na huko nikiomboleza kwa kudhulumiwa na adui yangu?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 Nakimbilia usalama kwako ee Mungu; kwa nini umenitupilia mbali? Yanini niende huko na huko nikiomboleza kwa kudhulumiwa na adui yangu?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 Nakimbilia usalama kwako ee Mungu; kwa nini umenitupilia mbali? Yanini niende huko na huko nikiomboleza kwa kudhulumiwa na adui yangu?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 Wewe ni Mungu ngome yangu. Kwa nini umenikataa? Kwa nini niendelee kuomboleza, nikidhulumiwa na adui?

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 Wewe ni Mungu ngome yangu. Kwa nini umenikataa? Kwa nini niendelee kuomboleza, nikiwa nimeonewa na adui?

Tazama sura Nakili




Zaburi 43:2
17 Marejeleo ya Msalaba  

Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa BWANA huchunguza mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, atakuwa nawe; ukimwacha, atakutupa milele.


Ee MUNGU Bwana, nguvu za wokovu wangu, Umenifunika kichwa changu siku ya vita.


BWANA ni nguvu zangu na ngao yangu. Moyo wangu umemtumaini, Nami nimesaidiwa; Basi, moyo wangu unashangilia, Na kwa wimbo wangu nitamshukuru.


Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri, Maana Wewe ndiwe ngome yangu.


Watesi wangu hunitukana mithili ya kuniponda mifupa yangu, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako?


Nitamwambia Mungu, mwamba wangu, Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?


Lakini umetutupa, umetufedhehesha, Wala huendi na majeshi yetu.


Usinitupe wakati wa uzee, Nguvu zangu zipungukapo usiniache.


Je! Bwana atatutupa milele na milele? Asiwe na fadhili kwetu kamwe?


Nimeteswa tangu ujana wangu na niko karibu kufa, Nimeumia kwa mapigo yako; nami nimekata tamaa.


Kwa kuwa BWANA hatawatupa watu wake, Wala hutauacha urithi wake,


BWANA ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.


bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watakimbia, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.


Mmoja ataniambia, Kwa BWANA, peke yake, iko haki na nguvu; naam, watu watamwendea yeye, na wote waliomkasirikia watatahayarika.


Nami nitawatia nguvu katika BWANA; nao watatembea huku na huko katika jina lake, asema BWANA.


Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.


Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo