Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 41:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

1 Heri amkumbukaye mnyonge; BWANA atamwokoa siku ya taabu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Heri mtu anayewajali maskini; Mwenyezi-Mungu atamwokoa wakati wa shida.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Heri mtu anayewajali maskini; Mwenyezi-Mungu atamwokoa wakati wa shida.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Heri mtu anayewajali maskini; Mwenyezi-Mungu atamwokoa wakati wa shida.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Mwenyezi Mungu atamwokoa wakati wa shida.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Heri mtu yule anayemjali mnyonge, bwana atamwokoa wakati wa shida.

Tazama sura Nakili




Zaburi 41:1
27 Marejeleo ya Msalaba  

Ametoa kwa ukarimu, na kuwapa maskini, Haki yake yakaa milele, Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.


Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini BWANA kutoka kwayo yote.


Hawataaibika wakati wa ubaya, Na siku za njaa watashiba.


Mchana kutwa hufadhili na kukopesha, Na mzao wake hubarikiwa.


Amdharauye mwenzake afanya dhambi; Bali amhurumiaye maskini ana heri.


Hasira ya mfalme ni kama wajumbe wa mauti; Lakini mtu mwenye hekima ataituliza.


Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.


Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.


Lakini nitakuokoa wewe katika siku hiyo, asema BWANA; wala hutatiwa katika mikono ya watu wale unaowaogopa.


maana sikuzote mnao maskini pamoja nanyi, na kila mpendapo mwaweza kuwatendea mema; lakini mimi hamko nami sikuzote.


Katika mambo yote nimewaonesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea.


ila neno moja tu walitutakia, tuwakumbuke maskini; nami neno lilo hilo nilikuwa na bidii kulifanya.


Ndugu, tunawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote.


Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu, na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia.


Maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.


Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi.


Basi mkwewe akamwuliza, Je! Umeokota wapi leo? Umefanya kazi wapi? Na abarikiwe yeye aliyekufahamu. Naye akamwarifu mkwewe ni nani ambaye alifanya kazi kwake, akasema, Yule mtu niliyefanya kazi kwake leo jina lake aitwa Boazi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo