Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 38:20 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

20 Naam, wakilipa mabaya kwa mema, Huwa adui zangu kwa kuwa nilifuata lililo jema.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

20 Hao wanaonilipa maovu kwa wema wangu, wananipinga kwa sababu natenda mema.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

20 Hao wanaonilipa maovu kwa wema wangu, wananipinga kwa sababu natenda mema.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

20 Hao wanaonilipa maovu kwa wema wangu, wananipinga kwa sababu natenda mema.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

20 Wanaolipa wema wangu kwa maovu hunisingizia ninapofuata lililo jema.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

20 Wanaolipa maovu kwa wema wangu hunisingizia ninapofuata lililo jema.

Tazama sura Nakili




Zaburi 38:20
18 Marejeleo ya Msalaba  

Uitoe nafsi yangu kifungoni. Nipate kulishukuru jina lako. Wenye haki watanizunguka, Kwa kuwa Wewe unanikirimu.


Uwatazame adui zangu, maana ni wengi, Na kwa namna wanavyonichukia kwa ukatili mwingi.


Wananilipa mabaya badala ya mema, Hata nafsi yangu ikaingia ukiwa.


Walio adui zangu bure wasinisimange, Wanaonichukia bila sababu wasining'ong'e.


Ikiwa nimemlipa mabaya Yeye aliyekaa kwangu salama; (Hasha! Nimemponya yeye Aliyekuwa mtesi wangu bila sababu;)


Je! Mabaya yalipwe badala ya mema? Maana wameichimbia nafsi yangu shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele zako, ili niseme mema kwa ajili yao, nikaigeuze ghadhabu yako isiwapate.


Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.


Yesu akawajibu, Kazi njema nyingi nimewaonesha, zitokazo kwa Baba; kwa ajili ya kazi ipi katika hizo mnanipiga kwa mawe?


Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?


si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake. Naye alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya, na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.


Ndipo Daudi akasema, Je! Watu wa Keila watanitia mimi na watu wangu mkononi mwake Sauli? BWANA akasema, Watakutia.


Ndipo wakaenda Keila, Daudi na watu wake, wakapigana na hao Wafilisti, wakateka nyara ng'ombe zao, na kuwaua uuaji mkuu. Hivyo Daudi akawaokoa watu wa Keila.


watu hao walikuwa boma kwetu usiku na mchana, wakati wote tulipokuwa nao tukiwachunga kondoo.


Basi Daudi alikuwa amesema, Hakika ni bure nilivyokuwa nikilinda nyikani yote aliyo nayo mtu huyu, asipotewe na kitu chochote cha mali yake yote; naye amenilipa mabaya badala ya mema.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo