Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 37:35 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

35 Nimemwona mtu asiye haki mkali sana, Akijieneza kama mwerezi wa Lebanoni.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

35 Nilimwona mwovu mdhalimu sana, alijiweka juu ya wote kama mierezi ya Lebanoni!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

35 Nilimwona mwovu mdhalimu sana, alijiweka juu ya wote kama mierezi ya Lebanoni!

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

35 Nilimwona mwovu mdhalimu sana, alijiweka juu ya wote kama mierezi ya Lebanoni!

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

35 Nimemwona mtu mwovu na mkatili akistawi kama mwerezi wa Lebanoni,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

35 Nimemwona mtu mwovu na mkatili akistawi kama mwerezi wa Lebanoni,

Tazama sura Nakili




Zaburi 37:35
16 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo Yoabu akasema, Siwezi kungoja na kusema nawe hivi. Akachukua mikuki mitatu midogo mkononi mwake, akamchoma Absalomu moyoni, alipokuwa bado hai katikati ya ule mwaloni.


Kisha vijana kumi, waliomchukulia Yoabu silaha zake wakamzunguka, wakampiga Absalomu, na kumwua.


Naye Hamani akawasimulia habari za fahari ya mali zake, na wingi wa watoto wake, na pia mambo yote ambayo mfalme amemfanikisha kwayo, na jinsi alivyompandisha cheo juu ya wakuu na watumishi wa mfalme.


Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi; Lakini mara niliyalaani maskani yake.


Umewapanda, naam, wametia mizizi, wanakua, naam, wanazaa matunda; katika vinywa vyao u karibu, bali katika mioyo yao u mbali.


Umefanana na nani, hivi katika utukufu na ukuu, kati ya miti ya Adeni? Lakini utashushwa pamoja na miti ya Adeni, hata pande za chini za nchi; utalala kati ya hao wasiotahiriwa; pamoja na hao waliouawa kwa upanga. Huyu ndiye Farao, na jamii yote ya watu wake, asema Bwana MUNGU.


Basi kimo chake kilitukuzwa kuliko miti yote ya shambani, na vitanzu vyake viliongezeka; matawi yake yakawa marefu, kwa sababu ya maji mengi, alipoyachipuza.


Ndipo atauelekeza uso wake kwenye ngome za nchi yake mwenyewe; lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.


Ndipo wakaingia waganga, na wachawi, na Wakaldayo, na wanajimu; nikawahadithia ile ndoto; wao wasiweze kunijulisha tafsiri yake.


Na nguvu zake zitakuwa nyingi mno, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe; naye ataharibu kiasi cha kustaajabisha watu, na kufanikiwa, na kutenda apendavyo; naye atawaangamiza hao walio hodari na watu watakatifu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo