Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 37:32 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

32 Mtu asiye haki humvizia mwenye haki, Na kutafuta jinsi ya kumwua.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

32 Mtu mwovu humvizia mtu mwema na kujaribu kumuua;

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

32 Mtu mwovu humvizia mtu mwema na kujaribu kumuua;

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

32 Mtu mwovu humvizia mtu mwema na kujaribu kumuua;

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

32 Watu waovu huvizia wenye haki, wakitafuta kuwaua;

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

32 Watu waovu huvizia wenye haki, wakitafuta kuwaua;

Tazama sura Nakili




Zaburi 37:32
18 Marejeleo ya Msalaba  

Basi akaiweka ile nguo kwake hata bwana wake aje nyumbani.


Akasema, Nendeni, mkamwangalie aliko, nipate kupeleka watu kwenda kumchukua. Akaambiwa ya kwamba, Tazama, yuko Dothani.


Asiye haki hunuia mabaya juu ya mwenye haki, Na kumsagia meno yake.


Je! Wataokoka kwa uovu wao? Ee Mungu, uwaangamize kwa hasira yako.


Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki; Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika;


Lakini mimi nilikuwa kama mwana-kondoo mpole, achukuliwaye kwenda kuchinjwa; wala sikujua ya kuwa wamefanya mashauri kinyume changu, wakisema, Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake, na tumkatilie mbali atoke katika nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.


Lakini wewe, BWANA, unajua mashauri yao yote juu yangu, ya kuniua; usiwasamehe uovu wao, wala usifute dhambi yao mbele za macho yako; bali wakwazwe mbele zako; uwatende mambo wakati wa hasira yako.


Maana nimesikia shutuma za watu wengi; hofu ziko pande zote. Rafiki zangu wote, wanaonivizia nisite, husema, Mshitaki, nasi tutamshitaki, huenda akahadaika, nasi tutamshinda, tutajilipiza kisasi kwake.


Ndipo wale watu wakasema, Hatutapata sababu ya kumshitaki Danieli huyo, tusipoipata katika mambo ya sheria ya Mungu wake.


wakimvizia, ili wapate neno litokalo kinywani mwake.


Ikawa alipoingia ndani ya nyumba ya mtu mmoja miongoni mwa wakuu wa Mafarisayo siku ya sabato, ale chakula, walikuwa wakimvizia.


Wakamviziavizia, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa watu wa haki, ili wamnase katika maneno yake, wapate kumtia katika enzi na mamlaka ya mtawala.


Na Waandishi na Mafarisayo walikuwa wakimvizia, ili waone kama ataponya siku ya sabato; kusudi wapate neno la kumshitakia.


lakini hila yao ikajulikana na Sauli. Wakamvizia malangoni mchana na usiku wapate kumwua.


Sauli akajaribu kumpiga Daudi hadi ukutani kwa mkuki wake, ila yeye akaponyoka kutoka mbele ya Sauli, nao huo mkuki akaupiga ukutani; naye Daudi akakimbia, akaokoka usiku ule.


Basi Daudi alikuwa akikaa nyikani ngomeni, akakaa katika nchi ya milima milima kwenye nyika ya Zifu. Naye Sauli alikuwa akimtafuta kila siku, lakini Mungu hakumtia mikononi mwake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo