Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 37:15 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

15 Upanga wao utaingia mioyoni mwao wenyewe, Na nyuta zao zitavunjika.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

15 Lakini panga zao zitawapenya wao wenyewe, na pinde zao zitavunjwavunjwa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

15 Lakini panga zao zitawapenya wao wenyewe, na pinde zao zitavunjwavunjwa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

15 Lakini panga zao zitawapenya wao wenyewe, na pinde zao zitavunjwavunjwa.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

15 Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe, na pinde zao zitavunjwa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

15 Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe, na pinde zao zitavunjwa.

Tazama sura Nakili




Zaburi 37:15
18 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Ahithofeli alipoona ya kuwa ushauri wake haukufuatwa, akatandika punda wake, akaondoka, akaenda nyumbani kwake, mjini mwake, akaitengeneza nyumba yake, akajinyonga; akafa, akazikwa kaburini mwa babaye.


Nao Wayahudi wengine waliokaa katika mikoa ya mfalme walikusanyika, wakayapigania maisha yao, wakajipatia raha mbele ya adui zao, wakawaua waliowachukia, watu elfu sabini na tano; lakini juu ya nyara hawakuweka mikono.


siku ambazo Wayahudi walijipatia raha mbele ya adui zao, na mwezi uliogeuzwa kwao kuwa furaha badala ya huzuni, na kuwa sikukuu badala ya kilio; wazifanye siku hizo ziwe za karamu na furaha, za kupeana zawadi na za kuwapa maskini tunu.


BWANA huzikomboa nafsi za watumishi wake, Wote wamkimbiliao hawatahukumiwa.


Uharibifu na umpate kwa ghafla, Na wavu aliouficha umnase yeye mwenyewe; Kwa uharibifu aanguke ndani yake.


Tulieni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.


Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari.


Ikawa alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisroki, mungu wake, Adrameleki na Shareza, wanawe, wakampiga kwa upanga; wakakimbilia nchi ya Ararati; naye Esar-hadoni, mwanawe, akatawala baada yake.


Kwa maana mwenye kuangamiza amefika kwake; Naam, amefika Babeli; Na mashujaa wake wametwaliwa; Pinde zao zimevunjika kabisa; Maana BWANA ni Mungu wa kisasi; Hakika yake yeye atalipa.


Tena itakuwa siku ile, nitauvunja upinde wa Israeli katika bonde la Yezreeli.


Nami siku hiyo nitafanya agano na wanyama wa mashamba kwa ajili yao, tena na ndege wa angani, tena na wadudu wa nchi; nami nitavivunja upinde na upanga na silaha vitoke katika nchi, nami nitawalalisha salama salimini.


Nao wataiharibu nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake; naye atatuokoa na Mwashuri, atakapoingia katika nchi yetu, na kukanyaga ndani ya mipaka yetu.


Pinde zao mashujaa zimevunjika, Na hao waliojikwaa wamepata nguvu.


Ndipo Sauli akamwambia yule mchukua silaha zake, Futa upanga wako, unichome nao; wasije watu hawa wasiotahiriwa wakanichoma, na kunisimanga. Lakini huyo mchukua silaha zake akakataa; kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akautwaa upanga wake, akauangukia.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo