Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 34:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

12 Ni nani atamaniye uzima na atakaye kuishi, Siku nyingi afurahie mema?

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

12 Je, watamani kufurahia maisha, kuishi maisha marefu na kufurahia mema?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

12 Je, watamani kufurahia maisha, kuishi maisha marefu na kufurahia mema?

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

12 Je, watamani kufurahia maisha, kuishi maisha marefu na kufurahia mema?

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,

Tazama sura Nakili




Zaburi 34:12
16 Marejeleo ya Msalaba  

Kusanyikeni, msikie, enyi wana wa Yakobo, Msikilizeni Israeli, baba yenu.


Kama sivyo, unisikilize mimi; Nyamaza, nami nitakufunza hekima.


Kumbuka ya kwamba maisha yangu ni upepo; Jicho langu halitaona mema tena.


Alikuomba uhai, ukampa, Muda mrefu wa siku nyingi, milele na milele.


Wengi husema, Nani atakayetuonesha mema? BWANA, utuinulie nuru ya uso wako.


Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonesha wokovu wangu.


Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzisikie kauli zangu.


Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Mkayaangalie maneno ya kinywa changu.


Kumcha BWANA ni mwanzo wa hekima; Na kumjua Mtakatifu ni ufahamu.


Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.


Moyoni mwangu nikapeleleza jinsi ya kuuburudisha mwili kwa mvinyo, na (moyo wangu ungali ukiniongoza kwa hekima) jinsi ya kushikana na upumbavu, hata niyaone yaliyo mema ya kuwafaa wanadamu, ili wayafanye hayo chini ya mbingu siku zote za maisha yao.


Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.


kumpenda BWANA, Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wako, na wingi wa siku zako; upate kukaa katika nchi BWANA aliyowaapia baba zako, Abrahamu, na Isaka, na Yakobo, kuwa atawapa.


upate kumcha BWANA, Mungu wako, kushika amri zake zote, na sheria zake, ninazokuamuru, wewe na mwanao, na mwana wa mwanao, siku zote za maisha yako; tena siku zako ziongezwe.


Lakini mimi, hasha! Nisimtende BWANA dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka


Tufuate:

Matangazo


Matangazo