Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 32:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

8 Nitakufundisha na kukuonesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Mungu asema: “Nitakufunza na kukuonesha njia unayopaswa kufuata. Nitakushauri kwa uangalifu mkubwa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Mungu asema: “Nitakufunza na kukuonesha njia unayopaswa kufuata. Nitakushauri kwa uangalifu mkubwa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Mungu asema: “Nitakufunza na kukuonesha njia unayopaswa kufuata. Nitakushauri kwa uangalifu mkubwa.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Nitakufundisha na kukuonesha njia utakayoiendea; nitakushauri na kukuangalia.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; nitakushauri na kukuangalia.

Tazama sura Nakili




Zaburi 32:8
16 Marejeleo ya Msalaba  

Nikainama, nikamsujudia BWANA, nikamtukuza BWANA, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, aliyeniongoza njiani, nimtwalie mwana wa bwana wangu binti wa ndugu yake.


Mungu ndiye ngome yangu yenye nguvu; Naye huwaongoza wakamilifu katika njia yake.


basi, usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo kuiendea; ukanyeshe mvua katika nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi wao.


Uniwezeshe kusikia fadhili zako asubuhi, Kwa maana nimekutumaini Wewe. Unifundishe njia nitakayoiendea, Kwa maana ninakuinulia nafsi yangu.


Ni nani amchaye BWANA? Atamfundisha katika njia anayoichagua.


Tazama, jicho la BWANA li kwao wamchao, Wazingojeao fadhili zake.


Njoni, enyi wana, mnisikilize, Nami nitawafundisha kumcha BWANA.


Mwanangu, usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike amri zangu.


BWANA, mkombozi wako, mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.


Hawataona njaa, wala hawataona kiu; joto halitawapiga, wala jua; kwa maana yeye aliyewarehemu atawatangulia, naam, karibu na chemchemi za maji atawaongoza.


Ikiwa lile wingu lilikawia, likikaa juu ya maskani siku mbili, au mwezi, au mwaka, wana wa Israeli walikaa katika kambi yao, wasisafiri;


Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo