Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 3:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

8 Wokovu ni wa BWANA; Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Mwenyezi-Mungu ndiwe uokoaye; uwape baraka watu wako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Mwenyezi-Mungu ndiwe uokoaye; uwape baraka watu wako.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Mwenyezi-Mungu ndiwe uokoaye; uwape baraka watu wako.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Kwa maana wokovu watoka kwa Mwenyezi Mungu. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Kwa maana wokovu watoka kwa bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

Tazama sura Nakili




Zaburi 3:8
22 Marejeleo ya Msalaba  

ila huyo alisimama katikati ya konde lile, akalipigania, akawaua Wafilisti; naye BWANA akafanya wokovu mkuu.


Mimi ni wako, uniokoe, Kwa maana nimejifunza mausia yako.


BWANA na awape watu wake nguvu; BWANA na awabariki watu wake kwa amani.


Umwangaze mtumishi wako Kwa nuru ya uso wako; Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.


Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi; Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu.


Jina lake na lidumu milele, Pindi ling'aapo jua, umaarufu wake uwepo; Mataifa yote na wabarikiwe katika yeye, Na kumwita heri.


Uwatie hofu, ee BWANA, Watu wa mataifa na wajitambue kuwa wao ni binadamu tu!


Farasi huwekwa tayari kwa siku ya vita; Lakini BWANA ndiye aletaye wokovu.


Mimi, naam, mimi, ni BWANA, zaidi yangu mimi hapana mwokozi.


Ni kweli, msaada haufai unaotazamiwa kutoka milimani, makutano yenye mshindo juu ya milima; ni kweli, wokovu wa Israeli ni katika BWANA, Mungu wetu.


Lakini mimi ni BWANA, Mungu wako tangu nchi ya Misri; wala hutamjua mungu mwingine ila mimi; wala zaidi ya mimi hakuna mwokozi.


Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; Nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa BWANA.


Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee BWANA, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao.


Mungu, akiisha kumfufua mtumishi wake Yesu, alimtuma kwenu ninyi kwanza, ili kuwabariki kwa kumwepusha kila mmoja wenu na maovu yake.


Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.


Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;


akisema, Hakika yangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza.


watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka.


Baada ya hayo nikasikia sauti kama sauti ya mikutano mikubwa, sauti kubwa mbinguni, ikisema, Haleluya; Wokovu na utukufu na nguvu zina Bwana Mungu wetu;


wakilia kwa sauti kuu wakisema, Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-kondoo.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo