Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 27:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Usinifiche uso wako, Usimkatalie mtumishi wako kwa hasira. Umekuwa msaada wangu, usinitupe, Wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Usiache kuniangalia kwa wema. Usinikatae kwa hasira mimi mtumishi wako; wewe umekuwa daima msaada wangu. Usinitupe wala usiniache, ee Mungu Mwokozi wangu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Usiache kuniangalia kwa wema. Usinikatae kwa hasira mimi mtumishi wako; wewe umekuwa daima msaada wangu. Usinitupe wala usiniache, ee Mungu Mwokozi wangu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Usiache kuniangalia kwa wema. Usinikatae kwa hasira mimi mtumishi wako; wewe umekuwa daima msaada wangu. Usinitupe wala usiniache, ee Mungu Mwokozi wangu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Usinifiche uso wako, usimkatae mtumishi wako kwa hasira; wewe umekuwa msaada wangu. Usinikatae wala usiniache, Ee Mungu Mwokozi wangu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Usinifiche uso wako, usimkatae mtumishi wako kwa hasira; wewe umekuwa msaada wangu. Usinikatae wala usiniache, Ee Mungu Mwokozi wangu.

Tazama sura Nakili




Zaburi 27:9
23 Marejeleo ya Msalaba  

Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa BWANA huchunguza mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, atakuwa nawe; ukimwacha, atakutupa milele.


Usinifiche uso wako siku ya shida yangu, Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi.


Maana siku zangu zinatoweka kama moshi, Na mifupa yangu inateketea kama kinga.


Nimefanya hukumu na haki, Usiniache mikononi mwao wanaonionea.


Ee BWANA, utanisahau hadi lini, hata milele? Hadi lini utanificha uso wako?


Ee BWANA, unijibu hima, roho yangu imelegea; Usinifiche uso wako, Nisifanane nao washukao shimoni.


Atapokea baraka kwa BWANA, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake.


Mbona unatuficha uso wako, Na kusahau kuonewa na kudhulumiwa kwetu?


Usinitenge na uso wako, Wala roho yako mtakatifu usiniondolee.


Wala usinifiche uso wako, mimi mtumishi wako, Maana mimi nimo taabuni, unijibu upesi.


Uikaribie nafsi yangu, uikomboe, Kwa sababu ya adui zangu unifidie.


Ee BWANA, Mungu wa wokovu wangu Mchana na usiku nimelia mbele zako.


BWANA asema hivi, Iko wapi hati ya talaka ya mama yenu, ambayo kwa hiyo niliachana naye? Au nimewauza ninyi kwa nani katika watu wanaoniwia? Ninyi mliuzwa kwa sababu ya maovu yenu; tena mama yenu ameachwa kwa sababu ya makosa yenu.


lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.


nami nitafanya agano la milele pamoja nao, kwamba sitageuka wala kuwaacha, ili niwatendee mema; nami nitatia kicho changu mioyoni mwao, ili wasiniache.


Msiwe na tabia ya kupenda fedha; muwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kamwe, wala sitakuacha.


Ndipo Samweli akatwaa jiwe, na kulisimamisha kati ya Mispa na Sheni, akaliita jina lake Ebenezeri, akisema, Hata sasa BWANA ametusaidia.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo