Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 27:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

5 Maana atanisitiri bandani mwake siku ya mabaya, Atanisitiri katika sitara ya hema yake, Na kuniinua juu ya mwamba.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Siku ya taabu atanificha bandani mwake; atanificha katika hema lake, na kunisalimisha juu ya mwamba.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Siku ya taabu atanificha bandani mwake; atanificha katika hema lake, na kunisalimisha juu ya mwamba.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Siku ya taabu atanificha bandani mwake; atanificha katika hema lake, na kunisalimisha juu ya mwamba.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Kwa kuwa siku ya shida, atanihifadhi salama katika maskani yake, atanificha uvulini mwa hema lake, na kuniweka juu kwenye mwamba.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Kwa kuwa siku ya shida, atanihifadhi salama katika maskani yake, atanificha uvulini mwa hema yake na kuniweka juu kwenye mwamba.

Tazama sura Nakili




Zaburi 27:5
33 Marejeleo ya Msalaba  

Akawako pamoja nao, amefichwa nyumbani mwa Mungu, miaka sita. Na Athalia akaitawala nchi.


Ee BWANA, kwa nini wasimama mbali? Kwani unajificha nyakati za shida?


Ndiwe sitara yangu na ngao yangu, Neno lako nimelingojea.


Nijapopitia katika shida, Unanilinda juu ya hasira ya adui zangu, Unaunyosha mkono wako, Na mkono wako wa kulia unaniokoa.


Unilinde kama mboni ya jicho, Unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako;


Miguu yangu anaifanya kuwa ya kulungu, Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.


Utawasitiri kutoka kwa fitina za watu Katika maficho ya kuwapo kwako; Utawaficha katika hema Na ushindani wa ndimi.


BWANA ahimidiwe; kwa maana amenitendea Fadhili za ajabu nilipozongwa kama mji wenye boma.


Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.


Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao watamtumainia BWANA.


Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.


Uniite siku ya mateso; Nitakuokoa, nawe utanitukuza.


Unirehemu, Ee Mungu, unirehemu mimi, Maana nafsi yangu imekukimbilia Wewe. Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako, Hadi misiba hii itakapopita.


Toka mwisho wa nchi nitakulilia ninapozimia moyo, Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda.


Kwa maana ulikuwa kimbilio langu, Ngome yenye nguvu adui asinipate.


Katika siku ya taabu yangu nilimtafuta Bwana; Mkono wangu ulinyoshwa usiku, bila kulegea; Nafsi yangu ilikataa kufarijika.


Juu ya watu wako wanafanya hila, Na kushauriana juu yao uliowaficha.


Aketiye mahali pa siri pake Aliye Juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.


Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;


Jina la BWANA ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.


BWANA, katika taabu zao walikwenda kwako; waliomba maombi mengi wakati adhabu yako ilipokuwa juu yao.


Njooni, watu wangu, ingia wewe ndani ya vyumba vyako, ukafunge mlango nyuma yako ujifiche kitambo kidogo, mpaka ghadhabu hii itakapopita.


Na mwanadamu atakuwa kama mahali pa kujificha na upepo, na mahali pa kujisitiri na dhoruba; kama mito ya maji mahali pakavu, kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi yenye uchovu.


Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku awakusanyavyo pamoja vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!


Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo