Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 25:13 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

13 Watafanikiwa maishani mwao; Na wazawa wao wataimiliki nchi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Mtu wa namna hiyo atafanikiwa daima, na wazawa wake watamiliki nchi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Mtu wa namna hiyo atafanikiwa daima, na wazawa wake watamiliki nchi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Mtu wa namna hiyo atafanikiwa daima, na wazawa wake watamiliki nchi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 Mtu huyo atafanikiwa maishani mwake, nao wazao wake watairithi nchi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 Mtu huyo atafanikiwa maishani mwake, nao wazao wake watairithi nchi.

Tazama sura Nakili




Zaburi 25:13
32 Marejeleo ya Msalaba  

Wazawa wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.


Jinsi zilivyo nyingi fadhili zako Ulizowawekea wakuchao; Ulizowatendea wakukimbiliao Mbele ya wanadamu!


Watashibishwa kwa unono wa nyumba yako, Nawe utawanywesha kutoka mto wa furaha zako.


Bali wenye upole watairithi nchi, Watajifurahisha kwa wingi wa amani.


Maana waliobarikiwa na BWANA watairithi nchi, Nao waliolaaniwa naye watakatiliwa mbali.


Mchana kutwa hufadhili na kukopesha, Na mzao wake hubarikiwa.


Wenye haki watairithi nchi, Nao watakaa humo milele.


Wewe umngoje BWANA, Uishike njia yake, Naye atakutukuza uirithi nchi, Utawaona Wasio haki wakiangamizwa.


Maana watenda mabaya watakatiliwa mbali, Bali wamngojao BWANA ndio watakaoirithi nchi.


Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono; Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.


Wazawa wa watumishi wake watairithi, Nao walipendao jina lake watakaa humo.


Bali kila anisikilizaye atakaa salama, Naye atatulia bila kuogopa mabaya.


Kumcha BWANA huelekea uhai; Atakaa ameshiba; hatajiliwa na ubaya.


Mwenye haki aendaye katika unyofu wake, Watoto wake wabarikiwa baada yake.


Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye BWANA atakuwa salama.


Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na BWANA, na watoto wao pamoja nao.


nami nitawapa moyo mmoja na njia moja, wapate kunicha sikuzote; kwa mema yao, na ya watoto wao baada yao;


BWANA, Mungu wako, yuko katikati yako shujaa awezaye kuokoa; Atakushangilia kwa furaha kuu, Atakutuliza katika upendo wake, Atakufurahia kwa kuimba.


Maana wema wake, jinsi ulivyo mwingi! Na uzuri wake, jinsi ulivyo mwingi! Nafaka itawasitawisha vijana wanaume, Na divai mpya vijana wanawake.


Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.


Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.


Akamnena Benyamini, Mpenzi wa BWANA atakaa salama kwake; Yuamfunika mchana kutwa, Naye hukaa kati ya mabega yake.


Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.


Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme uongo.


Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo