Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 23:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 na kuirudishia nafsi yangu nguvu mpya. Huniongoza katika njia sawa kwa hisani yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 na kuirudishia nafsi yangu nguvu mpya. Huniongoza katika njia sawa kwa hisani yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 na kuirudishia nafsi yangu nguvu mpya. Huniongoza katika njia sawa kwa hisani yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 hunihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 hunihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

Tazama sura Nakili




Zaburi 23:3
28 Marejeleo ya Msalaba  

Ili kurudisha roho yake itoke shimoni, Ili atiwe mwanga kwa mwanga wa walio hai.


Lakini akawaokoa kwa ajili ya jina lake, Ayadhihirishe matendo yake makuu.


Na Wewe, MUNGU, Bwana, unitendee kwa ajili ya jina lako, Kwa kuwa fadhili zako ni njema uniokoe.


Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea; Umtafute mtumishi wako; Kwa maana sikuyasahau maagizo yako.


Sheria ya BWANA ni kamilifu, Huiburudisha nafsi. Ushuhuda wa BWANA ni amini, Humtia hekima mtu asiye nayo.


Ndiwe mwamba wangu na ngome yangu; Kwa ajili ya jina lako uniongoze na unichunge.


Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri, Maana Wewe ndiwe ngome yangu.


Mtukuzeni BWANA pamoja nami, Na tuliadhimishe jina lake pamoja.


BWANA, uniongoze kwa haki yako, Kwa sababu yao wanaoniotea. Uinyoshe njia yako mbele ya uso wangu,


Ee Mungu, uniumbie moyo safi, Uifanye upya na kuithibiti roho yangu.


Unirudishie furaha ya wokovu wako; Unitegemeze kwa roho ya upendo.


Ee Mungu wa wokovu wetu, utusaidie, Kwa ajili ya utukufu wa jina lako. Utuokoe, utusamehe dhambi zetu, Kwa ajili ya jina lako.


Haki itakwenda mbele zake, Na kuzitayarishia hatua zake mapito.


Nimekufundisha katika njia ya hekima; Nimekuongoza katika mapito ya unyofu.


Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu.


Nitawaleta vipofu kwa njia wasiyoijua; katika mapito wasiyoyajua nitawaongoza; nitafanya giza kuwa nuru mbele yao; na mahali palipopotoka kuwa pamenyoka. Haya nitayatenda, wala sitawaacha.


Kwa maana nimeishibisha roho yenye uchovu, nami nimeiridhisha kila roho yenye huzuni.


Tazama, nitawaleta toka nchi ya kaskazini, na kuwakusanya katika miisho ya dunia, na pamoja nao watakuja walio vipofu, na hao wachechemeao, mwanamke mwenye mimba, na yeye pia aliye na uchungu wa kuzaa; watarudi huko, jeshi kubwa.


Lakini nilitenda kwa ajili ya jina langu, lisitiwe unajisi machoni pa mataifa, ambao niliwatoa mbele ya macho yao.


Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa.


Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo