Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 22:6 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

6 Lakini mimi ni mdudu wala si mtu, Nimedharauliwa na kupuuzwa na watu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 Lakini mimi ni mdudu tu, wala si mtu; nimepuuzwa na kudharauliwa na watu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 Lakini mimi ni mdudu tu, wala si mtu; nimepuuzwa na kudharauliwa na watu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 Lakini mimi ni mdudu tu, wala si mtu; nimepuuzwa na kudharauliwa na watu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.

Tazama sura Nakili




Zaburi 22:6
22 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Asa akamlilia BWANA, Mungu wake, akasema, BWANA, hapana kuliko wewe aliye wa kusaidia, kati yake yeye aliye hodari, na yeye asiye na nguvu; utusaidie, Ee BWANA, Mungu wetu; kwa kuwa sisi twakutegemea wewe, na kwa jina lako tumekuja juu ya jamii kubwa hii. Ee BWANA, wewe ndiwe Mungu wetu, asikushinde mwanadamu.


Seuze mtu, aliye mdudu! Na mwanadamu, ambaye ni buu!


Naam, wakungojao hawataaibika hata mmoja; Wataaibika watendao uhaini bila sababu.


Nimekukimbilia Wewe, BWANA, Nisiaibike milele. Kwa haki yako uniponye,


Kwa sababu ya watesi wangu nimelaumiwa, Naam, hasa kwa jirani zangu; Na kitu cha kutisha kwa rafiki zangu; Wanaoniona njiani wananikimbia.


Adui zangu wananitaja kwa maneno mabaya, Atakufa lini, jina lake lipotee?


Wanijuao umewatenga nami; Umenifanya kuwa chukizo kwao; Nimefungwa wala siwezi kutoka.


Usiogope, Yakobo uliye mdudu, nanyi watu wa Israeli; mimi nitakusaidia, asema BWANA, na mkombozi wako ni Mtakatifu wa Israeli.


BWANA, mkombozi wa Israeli, Mtakatifu wake, amwambia hivi yeye anayedharauliwa na wanadamu; yeye anayechukiwa na taifa hili; yeye aliye mtumishi wao watawalao; Wafalme wataona, watasimama; wakuu nao watasujudu; kwa sababu ya BWANA aliye mwaminifu, Mtakatifu wa Israeli aliyekuchagua.


Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.


Na amwelekezee yule ampigaye shavu lake; Ashibishwe mashutumu.


Mwana wa Adamu alikuja, akila na kunywa, wakasema, Mlafi huyu, na mlevi, rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi! Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake.


Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo.


Wayahudi wakastaajabu wakisema, Amepataje huyu kujua elimu, ambaye hakusoma?


Mkutano wakajibu, Ama! Una pepo! Ni nani anayetafuta kukuua?


Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Je! Sisi hatusemi vema ya kwamba wewe u Msamaria, nawe una pepo?


Kwa ajili hii Yesu naye, ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa nje ya lango.


Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo