Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 20:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

8 Wao wameinama na kuanguka, Bali sisi tumeinuka na kusimama.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Hao watajikwaa na kuanguka; lakini sisi tutainuka na kusimama imara.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Hao watajikwaa na kuanguka; lakini sisi tutainuka na kusimama imara.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Hao watajikwaa na kuanguka; lakini sisi tutainuka na kusimama imara.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Wao wameshushwa chini na kuanguka, bali sisi tunainuka na kusimama imara.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Wao wameshushwa chini na kuanguka, bali sisi tunainuka na kusimama imara.

Tazama sura Nakili




Zaburi 20:8
17 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa vinywa vya wajumbe wako umemshutumu Bwana, ukasema, Kwa wingi wa magari yangu nimepanda juu ya vilele vya milima, mpaka mahali pa ndani pa Lebanoni. Nami nitaikata mierezi yake mirefu, na misonobari yake mizuri; nami nitaingia ndani ya makazi yake yaliyo mbali sana, na msitu wa shamba lake lizaalo sana.


Asa akatoka kukutana naye, wakapanga vita Maresha bondeni mwa Sefatha.


Naye Asa akamlilia BWANA, Mungu wake, akasema, BWANA, hapana kuliko wewe aliye wa kusaidia, kati yake yeye aliye hodari, na yeye asiye na nguvu; utusaidie, Ee BWANA, Mungu wetu; kwa kuwa sisi twakutegemea wewe, na kwa jina lako tumekuja juu ya jamii kubwa hii. Ee BWANA, wewe ndiwe Mungu wetu, asikushinde mwanadamu.


Maana niliona haya kumwomba mfalme kikosi cha askari na wapanda farasi, ili kutusaidia juu ya adui njiani; kwa maana tulikuwa tumesema na mfalme, tukinena, Mkono wa Mungu u juu ya watu wote wamtafutao, kuwatendea mema; bali uweza wake na ghadhabu yake ni juu ya wote wamkataao.


Msaada wetu u katika jina la BWANA, Aliyeziumba mbingu na nchi.


Wamtumainio BWANA ni kama mlima Sayuni, Ambao hautikisiki, wakaa milele.


Mfalme haokolewi kwa jeshi lake kubwa, Wala shujaa haokoki kwa kuwa na nguvu nyingi.


Farasi hafai kitu kwa wokovu, Wala hamponyi mtu kwa wingi wa nguvu zake.


Farasi huwekwa tayari kwa siku ya vita; Lakini BWANA ndiye aletaye wokovu.


Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha.


Usifurahi juu yangu, Ee adui yangu; niangukapo, nitasimama tena; nikaapo gizani, BWANA atakuwa nuru kwangu.


Nao wakatoka nje, wao na mjeshi yao yote pamoja nao, watu wengi mno, kama mchanga ulio ufuoni mwa bahari kwa wingi, pamoja na farasi na magari mengi sana.


Na waangamie vivyo hivyo adui zako wote, Ee BWANA. Bali wao wampendao na wawe kama jua hapo litokapo kwa nguvu zake. Nayo nchi ikastarehe miaka arubaini.


Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la BWANA wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo