Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 19:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

8 Maagizo ya BWANA ni ya adili, Huufurahisha moyo. Amri ya BWANA ni safi, Huyatia macho nuru.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

8 Kanuni za Mwenyezi-Mungu ni sawa, huufurahisha moyo; amri ya Mwenyezi-Mungu ni safi, humwelimisha mtu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

8 Kanuni za Mwenyezi-Mungu ni sawa, huufurahisha moyo; amri ya Mwenyezi-Mungu ni safi, humwelimisha mtu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

8 Kanuni za Mwenyezi-Mungu ni sawa, huufurahisha moyo; amri ya Mwenyezi-Mungu ni safi, humwelimisha mtu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

8 Maagizo ya Mwenyezi Mungu ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Mwenyezi Mungu huangaza, zatia nuru machoni.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

8 Maagizo ya bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za bwana huangaza, zatia nuru machoni.

Tazama sura Nakili




Zaburi 19:8
44 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa sababu Abrahamu alisikia sauti yangu, akayahifadhi maagizo yangu, na amri zangu, na hukumu zangu, na sheria zangu.


na sheria, na hukumu, na torati, na amri, alizowaandikia, hizo ndizo mtakazozishika na kuzifanya hata milele; wala msiche miungu mingine.


Na watu wote wakaenda zao kula na kunywa, na kuwapelekea watu sehemu, na kufanya furaha nyingi, kwa sababu walikuwa wameyafahamu maneno yale waliyohubiriwa.


Tena ulishuka juu ya mlima Sinai, ukasema nao toka mbinguni, ukawapa hukumu za haki, na sheria za kweli, na amri nzuri na maagizo;


Ili wazishike amri zake, na kuzitii sheria zake. Haleluya.


Matendo ya mikono yake ni kweli na hukumu, Maagizo yake yote ni amini,


Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.


Ee BWANA, umehimidiwa, Unifundishe amri zako.


Nimefanya hukumu na haki, Usiniache mikononi mwao wanaonionea.


Maana nayafuata mausia yako yote, kuwa ya adili, Kila njia ya uongo naichukia.


Kufafanuliwa kwa maneno yako kunatia nuru, Na kumfahamisha mjinga.


Nimeifurahia njia ya shuhuda zako Kana kwamba ni mali mengi.


Taabu na dhiki zimenipata, Maagizo yako ni furaha yangu.


Nitajifurahisha sana kwa amri zako, Sitalisahau neno lako.


Midomo yangu na itoe sifa, Kwa kuwa unanifundisha mausia yako.


Shuhuda zako nazo ndizo furaha yangu, Na washauri wangu.


Tazama, nimeyatamani mausia yako, Unihuishe kwa haki yako.


Amri zako zimekuwa nyimbo zangu, Katika nyumba yangu ya ugenini.


Moyo wangu na uwe mkamilifu katika amri zako, Nisije mimi nikaaibika.


Kama sheria yako isingalikuwa furaha yangu, Hapo ningalipotea katika mateso yangu.


Maneno ya BWANA ni maneno safi, Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi; Iliyosafishwa mara saba.


Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti.


Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.


Shuhuda zako ni amini sana; Utakatifu ndio uifaao nyumba yako, Ee BWANA, milele na milele.


wakiwa na neno, hunijia; nami naamua kati ya mtu na mwenziwe, nami nawajulisha amri za Mungu, na sheria zake.


Kwa kuwa BWANA huwapa watu hekima; Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu;


Kila neno la Mungu limehakikishwa; Yeye ni ngao yao wamwaminio.


Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru, Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.


Wewe wamlaki yeye afurahiaye yaliyo haki na kuyatenda, watu wale wakukumbukao katika njia zako; tazama, ulikuwa na hasira, nasi tulitenda dhambi; tumekuwa katika dhambi kwa muda mrefu, nasi Je! Tutaokolewa?


Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na maneno yako yalikuwa ni furaha kwangu, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee BWANA, Mungu wa majeshi.


Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda.


kwa sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria; kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya sheria.


Kwa maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani,


Tusemeje, basi? Torati ni dhambi? La hasha! Lakini singalitambua dhambi ila kwa sheria; kwa kuwa singalijua kutamani, kama torati isingalisema, Usitamani.


Maana mimi kwa njia ya sheria niliifia sheria ili nimwishie Mungu.


Basi je! Torati haipatani na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa kuwa, kama ingalitolewa sheria iwezayo kuhuisha, hakika haki ingalipatikana kwa sheria.


nawe utafurahi mbele ya BWANA, Mungu wako, wewe na mwana wako na binti yako, na mtumwa wako na mjakazi wako, na Mlawi aliye ndani ya malango yako, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio katikati yako, katika mahali atakapochagua BWANA, Mungu wako, apakalishe jina lake.


nawe utafurahi katika sikukuu yako, wewe, na mwanao, na binti yako, na mtumwa wako, na mjakazi wako, na Mlawi, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo