Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 19:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

7 Sheria ya BWANA ni kamilifu, Huiburudisha nafsi. Ushuhuda wa BWANA ni amini, Humtia hekima mtu asiye nayo.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

7 Sheria ya Mwenyezi-Mungu ni kamilifu, humpa mtu uhai mpya; masharti ya Mwenyezi-Mungu ni thabiti, huwapa hekima wasio na makuu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

7 Sheria ya Mwenyezi-Mungu ni kamilifu, humpa mtu uhai mpya; masharti ya Mwenyezi-Mungu ni thabiti, huwapa hekima wasio na makuu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

7 Sheria ya Mwenyezi-Mungu ni kamilifu, humpa mtu uhai mpya; masharti ya Mwenyezi-Mungu ni thabiti, huwapa hekima wasio na makuu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

7 Torati ya Mwenyezi Mungu ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Mwenyezi Mungu ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

7 Torati ya bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.

Tazama sura Nakili




Zaburi 19:7
41 Marejeleo ya Msalaba  

Je! Sivyo ilivyo nyumba yangu mbele za BWANA? Kwa kuwa amefanya nami agano la milele; Ina taratibu katika yote, ni thabiti, Maana ni wokovu wangu wote, na shauku langu lote.


Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu,


Matendo ya mikono yake ni kweli na hukumu, Maagizo yake yote ni amini,


Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.


Shuhuda zako nimezifanya urithi wa milele, Maana ndizo changamko la moyo wangu.


Kufafanuliwa kwa maneno yako kunatia nuru, Na kumfahamisha mjinga.


Nimeifurahia njia ya shuhuda zako Kana kwamba ni mali mengi.


Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako, Ya kuwa umeziweka zikae milele.


Shuhuda zako nazo ndizo furaha yangu, Na washauri wangu.


Sheria ya kinywa chako ni njema kwangu, Kuliko maelfu ya dhahabu na fedha.


Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.


Mungu, njia yake ni kamilifu, Ahadi ya BWANA imehakikishwa, Yeye ndiye ngao yao. Wote wanaomkimbilia.


Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.


Shuhuda zako ni amini sana; Utakatifu ndio uifaao nyumba yako, Ee BWANA, milele na milele.


Kuwapa wajinga werevu, na kijana maarifa na tahadhari;


Ufunge huo ushuhuda, ukaitie mhuri sheria kati ya wanafunzi wangu.


Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi kulingana na neno hili, bila shaka kwa hao hakuna asubuhi.


Mnayachunguza maandiko kwa sababu mnadhani kuwa ndani yake ninyi mna uzima wa milele; na maandiko yayo hayo ndiyo yanayonishuhudia.


Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.


Wala msifuate kanuni za dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.


Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya Maandiko tupate kuwa na tumaini.


Kwafaa sana kwa kila njia. Kwanza kwa kuwa wamekabidhiwa mausia ya Mungu.


Yeye Mwamba, kazi yake ni kamilifu; Maana, njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, asiye na uovu, Yeye ndiye mwenye haki na adili.


Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.


Basi usiuonee haya ushuhuda wa Bwana wetu, wala usinionee haya mimi mfungwa wake, bali uvumilie mabaya pamoja nami kwa ajili ya Injili, kwa uweza wa Mungu;


Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye mhuri huu, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila aliitaye jina la Bwana na auache uovu.


Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka.


Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda kulingana na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.


Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mtumishi mwenzako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo