Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Zaburi 18:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

9 Aliziinamisha mbingu akashuka, Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Aliinamisha anga, akashuka chini; na wingu jeusi chini ya miguu yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Aliinamisha anga, akashuka chini; na wingu jeusi chini ya miguu yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Aliinamisha anga, akashuka chini; na wingu jeusi chini ya miguu yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.

Tazama sura Nakili




Zaburi 18:9
17 Marejeleo ya Msalaba  

Aliziinamisha mbingu akashuka; Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.


Mungu wetu atakuja wala sio kimya kimya, Moto utakula mbele zake, na tufani yavuma sana ikimzunguka pande zote.


Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake, Mwimbieni wimbo yeye apitaye katika mawingu, Jina lake ni YAHU; Shangilieni mbele zake.


Moto hutangulia mbele zake, Nao huwateketeza watesi wake pande zote.


Mlima wa Sinai wote pia ukatoa moshi, kwa sababu BWANA alishuka katika moto; na ule moshi wake ukapanda juu kama moshi wa tanuri, mlima wote ukatetemeka sana.


Inueni macho yenu mbinguni, mkaitazame nchi chini; maana mbingu zitatoweka kama moshi, na nchi itachakaa kama vazi, nao wakaao ndani yake watakufa kadhalika; bali wokovu wangu utakuwa wa milele, na ukombozi wangu hautakoma kamwe.


Maana BWANA atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto.


Naye BWANA atanguruma toka Sayuni, atatoa sauti yake toka Yerusalemu; na mbingu na nchi zitatetemeka; lakini BWANA atakuwa kimbilio la watu wake, na ngome ya wana wa Israeli.


Lakini mara tu, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka kutoka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;


Na ilipokuwa saa sita, palikuwa na giza juu ya nchi yote, hadi saa tisa.


Yesu akajibu, akamwambia, Nifanyalo wewe hujui sasa; lakini utalifahamu baadaye.


Hapana aliyefanana na Mungu, Ee Yeshuruni, Ajaye amepanda juu ya mbingu ili akusaidie. Na juu ya mawingu katika utukufu wake.


ambaye sauti yake iliitetemesha nchi wakati ule; lakini sasa ameahidi akisema, Mara moja tena nitatetemesha si nchi tu, bali na mbingu pia.


Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.


Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo