Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 17:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

4 Kuhusu matendo ya wanadamu; Kwa neno la midomo yako Nimejiepusha na njia za wenye jeuri.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 Kuhusu matendo watendayo watu; mimi nimeitii amri yako, nimeepa njia ya wadhalimu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 Kuhusu matendo watendayo watu; mimi nimeitii amri yako, nimeepa njia ya wadhalimu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 Kuhusu matendo watendayo watu; mimi nimeitii amri yako, nimeepa njia ya wadhalimu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.

Tazama sura Nakili




Zaburi 17:4
20 Marejeleo ya Msalaba  

Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia ikajaa dhuluma.


BWANA akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu siku zote.


Sembuse mtu ambaye ni mwenye kuchukiza na uchafu, Mwanadamu anywaye uovu kama anywavyo maji!


Ikiwa kama mwanadamu nimeyafunika makosa yangu, Kwa kuuficha uovu wangu kifuani mwangu;


Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Mwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.


Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.


Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.


Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.


kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?


Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;


Kwa kupenda kwake mwenyewe alituzaa sisi kwa neno la kweli, tuwe kama limbuko la viumbe vyake.


Muwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka zunguka, akitafuta mtu ammeze.


Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.


Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kigiriki analo jina lake Apolioni.


Hasha! Nisiunyoshe mkono wangu juu ya masihi wa BWANA; lakini sasa tafadhali twaa hili fumo lililo kichwani pake, na hili gudulia la maji, nasi twende zetu.


Lakini Daudi akamwambia Abishai, Usimwangamize; kwani ni nani awezaye kuunyosha mkono wake juu ya masihi wa BWANA, naye akawa hana hatia?


Tufuate:

Matangazo


Matangazo